Picha 8 Exclusive : "They shouted coward at you this afternoon..".. Waziri Mkuu wa Uingereza apitia machungu ya uunguaji Grenfell..' aonyeshwa picha 8 za kutisha za 'sweeping fire' ulivyoimaliza Grenfell Tower !

Waziri Mkuu Mteule Bi Theresa May wa Uingereza, jana alipokea ripoti maalum kutoka vyombo vya usalama zikiwemo 'picha 8 za siri' za jinsi moto huo wa ajabu ulivyotumia masaa 4 tu kuitekeza Grenfell Tower... 'the flames rapidly raced up the building soon after 1.30am, and by 5.16am.. the tower was all consumed.." alieleza mmoja wa maofisa kutoka vikosi maalum.


Awali bi May alikumbana na maswali ya kutamausha alipohudhuria kipindi kimoja cha Televisheni ambapo mwandishi wa BBC Emily Mailtis alitaka kujua amechukua hatua gani kama Waziri Mkuu tokea tukio la moto wa Grenfell..

Bi May amekuwa akikumbana na upinzani mkali kufuatia hatua yake ya siku ya Alhamis alivyotembelea eneo la tukio na kukataa kuonana na wahasiriwa wa mkasa wa Grenfell waliokuwa wakihangaikia mustakabali wao... kama ilivyokuwa kwa Meya wa London Bw. Khan, askari wa Usalama walilazimika kumkimbizia Bi May kwenye gari lake aina ya Jeep kuepuka mashambulizi ya umma wenye hasira..

Hadi sasa mbali na majeruhi na maiti 30 zilizopatikana, bado kuna shakashaka ya watu wengine 70 ambao hawaonekani miongoni mwa wakaazi 600 wa kwenye appartments 120 za jengo hilo kubwa la Grenfell, na huenda nao wameteketea kabisa wakiwapo watoto wadogo...

Katika mahojiano hayo hapo awali Bi Mailtis alimwambia Bi May.. "You misread the public mood on this one,.. you misread the anger the people felt about this.. The shouted coward at you this afternoon..'
Waziri Mkuu May alielezwa wakazi wa jengo hilo walionusurika wamepoteza kila kitu yakiwemo makazi na haijulikani mustakbali wao..










About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search