Top news: Serikali Yaongeza Wiki mbili Kodi ya Majengo.. #share Ewura "yashusha neema" kwa wenye Magari.. ni kuanzia 01/07/2017

Mamlaka ya Mapato (TRA) nchini imeongeza siku 14 za ulipaji wa kodi ya majengo ili kuwasaidia wale ambao wamechelewa kukamilisha mchakato huo.
Hayo yameelezwa leo Ijumaa (Juni 30) na Meneja wa TRA, Temeke, Warioba Kenere, ikiwa ni siku ya mwisho iliyotangazwa na mamlaka hiyo kwa wananchi kulipa kodi ya majengo.
Ni jana Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi wa TRA wa Richard kayombo alitahadharisha kuwa hawataongeza muda wa kulipa kodi hizo na badala yake ambao hawatalipa kufikia tarehe ya mwisho iliyowekwa watatakiwa kulipa faini ya Sh 75,000.
Serikali imeongeza wiki 2 kwa wananchi kukamilisha ulipaji kodi ya majengo. Kaimu Meneja wa TRA, Temeke Warioba Kerene asema.— CloudsMediaLive (@CloudsMediaLive) June 30, 2017
— Zitto Kabwe Ruyagwa (@zittokabwe) June 30, 2017
Waziri wa Afya amesema uchunguzi umebaini Mwanamke aliyedai kuibiwa mtoto pacha Hospitali ya Temeke, alikuwa na mimba ya mtoto 1#JFLeo pic.twitter.com/pbyWHp039G— Jamii Forums (@JamiiForums) June 30, 2017
Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji(EWURA) yatangaza kushuka bei za Dizeli, Petroli na Mafuta ya Taa kuanzia July 1, 2017#JFLeo pic.twitter.com/dcN7fLmhTM— Jamii Forums (@JamiiForums) June 30, 2017
Tamko la pamoja la Asasi za kiraia kuhusu kuwapa fursa— HakiElimu (@HakiElimu) June 30, 2017
wasichana kurudi shuleni baada ya kujifungua lipo hapa https://t.co/QaRePZr4eQ pic.twitter.com/w2A3Nm7vD7
Nawaomba wananchi wenye maoni/maboresho juu ya miswada (rasilimali+madini) iliyowasilishwa bungeni wanitumie kwa: mbungekibamba@gmail.com pic.twitter.com/IuIbsFtAvC— MNYIKA John John (@jjmnyika) June 30, 2017
Amani: kulikuwa na taarifa nina mtoto na AY, habari hizo hazina ukweli. Tulikuwa wapenzi miaka 10 iliyopita ila hatukufanikiwa kupata mtoto. pic.twitter.com/iMuqgvFAaK— Swahili Times (@swahilitimes) June 30, 2017
Nimekuwa nikipinga Hati za dharura kwenye miswada tata TU. Miswada hii (mimi) naiona siyo tata. Imesheheni tulivyopigania miaka yote. #Uhuru pic.twitter.com/U83nBcXg4A— Irenei Kiria (@IreneiKiria) June 30, 2017
Tutembelee katika maonyedho ya Sabasaba ambapo utaweza kupata huduma zote za kibenki kupitia tawi linalotembea(mobile branch)#UlipoTupo pic.twitter.com/y73qlSDod3— CRDB Bank Plc (@CRDBBankPlc) June 30, 2017
Ujerumani yahalalisha ndoa za jinsia moja baada ya wabunge wengi kuunga mkono muswada ambao Kansela Merkel aliupinga. pic.twitter.com/gr3LKokLtZ— Swahili Times (@swahilitimes) June 30, 2017
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetoa bei kikomo za mafuta ambapo petroli, diseli na mafuta ya taa yamepungua kwa sh. 37 kwa lita sawa na asilimia 1.81 huku mkoa wa Tanga bei ikipanda.
Aidha, Ewura imesema kushuka kwa bei kutasababisha bei ya petroli kuwa sh.2014 , dizeli sh.1874 na mafuta ya taa sh. 1806.
Akizungumza jana na waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi wa Ewura, Godwin Samwel alisema bei hizo zitaanza kutumika Julai mosi mwaka huu na kwamba kupungua huko kumetokana na kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia na gharama za usafirishaji mafuta.
Alisema bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya aina zote ikiwa ni petroli, dizeli na mafuta ya taa zimepungua ikilinganishwa na tolea lililopita la Juni 7 ambapo kwa mwezi utakao anza wa saba bei za rejareja dizeli na mafuta ya taa zimepungua kwa asilimia 1.81
Hata hivyo alieleza kwa kulinganisha na toleo la mwezi uliopita bei za jumla za petroli, dizeli na mafuta ya taa nazo zimepungua kwa asilimia 1.92 hii ni kwa lita 37 ambapo lita 13 ni asilimia 0.77 na lita 18 ambayo ni sawa na asilimia 1.10.
Aidha bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya petroli na dizeli zimeongezeka kwa Mkoa wa Tanga ilikilinganishwa na toleo lililopita ambapo ongezeko hilo limetokana na mabadiliko ya soko la mafuta katika soko la dunia.
"Kutokana na kutopokea mzigo mpya wa mafuta ya taa katika Bandari ya Tanga kwa mwezi Juni mwaka huu wamiliki wa vituo vya mafuta Mkoa wa Tanga wanashauriwa kununua mafuta hayo kutoka Dar es Salaam" alisema
Alisema katika Bunge la bajeti lilanaloendelea Dodoma lilipitisha muswada wa mabadiliko ya ushuru kwa bidhaa za mafuta ya petroli dizeli na mafuta ya taa ambapo shilingi 40 kwa lita moja zimeongezwa kwenye viwango vya awali vya ushuru.
"Kwa mujibu wa sheria ya mafuta ya mwaka 2015, bei za bidhaa za mafuta ya petroli zitaendelea kupangwa na soko na tutaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta" alisema.
Aidha alisema vituo vyote mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za mafuta katika mabango yanayoonekana na kuonesha bei ya mafuta, punguzo, kwenye vivutio vya bioashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika.
Hata hivyo alisema wanunuzi wametakiwa wahahakishe wanapata stakabadhi ya ,alipo inayoonesha jina la kituo ,tarehe na aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwea kil alita ambapo itatumika kama kidhibiti cha manunuzi.
No comments:
Post a Comment