bREAKING nEWS: Siku moja baada ya 'kuwanyoosha' wadau wa Camera,.. RC Makonda 'afanya kufuru' nyengine Dar.. #share..

Ikiwa ni siku moja tu tokea ukimya wake wa muda mrefu kwenye vyombo vya habari, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam, 'Commandat RC Field Marshall' Paul Makonda, leo amefanya 'surprise ya mwaka' alipoinuka kuwahutubia maelfu kwa mamia ya wakazi wa Jiji katika Tamasha maalum la ... KOMAA SUPER SHOW lililoandaliwa na kituo kimoja maarufu cha Radio cha EFM cha Jijini Dar es Salaam.


Hatua hii ya EFM inaonekana ni mabadiliko makubwa tokea kituo hicho kilipomkaribisha RC katika hafla ya mazishi ya muandaaji vipindi wa efm, Bikira wa kisukuma wiki mbili zilizopita kisha kumuwekea 'pazia' kwenye kamera zake.
Itakumbukwa vyombo vya habari viliweka msimamo chini ya Jukwaa la TEF la kutochapa habari za RC Makonda kufuatia sakata la 'uvamizi wa Clouds, ze pipo station..'
Matukio360 imekutupia picha tano za RC Makonda na muitikio wa wana-Darisalama katika tamasha la leo...

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search