tETESI zA uSAJILI bARANI uLAYA: Usajili wa Neymar kwenda PSG wamvuruga kichwa Valverde wa Barcelona #share..

Kocha wa Klabu ya  Barcelona Ernesto Valverde amesisitiza kuwa Neymar yupo katika mipango yake msimu ujao na kukanusha tetesi za dili la mchezaji huyo kuhamia PSG kwa dau la £195m.


Kocha huyo aliulizwa maswali kuhusu mipango yake juu ya mchezaji huyo wakati huu ambapo klabu ya Paris St Germain's iko tayari kuvunja rekodi ya usajili kwa dau la £195m.

Amesema: 'Kila mara najaribu kuzungumzia kuhusu masuala yanayotokea kuliko masuala ambayo yanayoweza kutokea. Tunakwenda kusubiri. Kwa mtazamo wangu tunaye Neymar kwenye timu yetu, tunamtegemea, tunapaswa kuona,” amesema.

“Sitaki kutafakari kuhusu Neymar. Ninamwona katika sehemu ile ile ninayomuona hivi sasa – uwanjani na sisi,” amesisitiza.


Katika siku za hivi Neymar da Silva Santos Júnior, (25) amekuwa akihusishwa kwa kiasi kikubwa kuhamia klabu ya PSG ya nchini Ufaransa hadi jana taarifa zilikuwa zinadai kuwa ata saini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo.

chanzo: Mail Online

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search