eXCLUSIVE ya matukio360 na Hashim Rungwe kudai eti CUF 'inatafunwa na wenye njaa'.. atoa dira ya kuua mgogoro.. #share

MWENYEKITI wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chauma) Hashim Rungwe, amesema mgogoro unaoendelea ndani ya Chama cha Wananch CUF ni kuwepo kwa kundi linaloangalia maslahi binfsi ya matumbo yao.


Kauli hiyo Rungwe ameitoa leo wakati akizungumza na Matukio360, amesema njaa ndiyo imeifikisha CUF katika sakata hilo na kuonyesha kusikitishwa na jinsi chama hicho kikongwe nchini kwa sasa kinavyokosa mwelekeo wa kisiasa.

“Mgogoro wa CUF wa sasa unasababishwa na njaa, kwa maana ya kwamba kuna kundi, linachoangalia sana ni maslahi ya matumbo yao, hawana ajenda yani ya maana ya kuleta mabadiliko,” alisema Rungwe.

Aidha ameeleza kuwa kundi hilo linapambana na kundi la pili ambalo limejidhatiti kwa ajili ya kuleta mabadiliko ya kweli na kutotanguliza njaa.

Amebanisha kuwa kundi hilo la pili kama lingekuwa na maslahi binafsi lingekuwa limetulia kwani fursa ilikuwa ya kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar lakini limekataa na kusema kuwa linataka kuendelea na mapambano ya kubadilisha mfumo uliopo katika serikali.

Rungwe ameonyesha masikitiko juu ya sakata hilo na kusema ni bahati mbaya kwa kuwepo kwa pande hizo mbili ambazo zinasigana. Alibainisha kuwa katika pande hizo kuna upande ambao umeonyesha kuungwa mkono na watu wenge huku mwingine ukiungwa na wachache.

Kutokana na hali hiyo ameshauri wanaodhani kutotendewa haki kwa sababu ya sakata hilo akitolea mfano wabunge waliovuliwa uanachama kwenda mahakamani kwani ndiyo mahali pekee wanapoweza pata haki yao.

Na: Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search