tOP nEWS:: Kim arusha kombora la masafa marefu.. asema sasa ana uwezo 'kumpumulia mmarekani' wakati wowote akitaka.. #share

Korea Kaskazini imesema kuwa imefanikiwa kufanyia jaribio kombora lake la masafa marefu ICBM, wakitaja kuwa onyo kali kwa Marekani.


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un alisema kuwa jaribio hilo lilibaini kwamba marekani yote ipo katik radara ya Korea Kakazini na sasa inaweza kushambuliwa, vyombo vya habari vimeripoti.

Jaribio la kombora hilo linajiri wiki tatu baada ya jaribio la kombora la kwanza la masafa marefu la Korea Kaskazini.

Rais wa Marekani Donald Trump amelitaja jaribio hilo kuwa la kijinga na kitendo cha hatari kilichotekelezwa na utawala wa Korea Kaskazini .

China pia imeshutumu jaribio hilo huku ikitaka pandfe husika zilizo na waiwasi kujizuia ili kutoendeleza wasiwasi zaidi.

Ikithibtisha kurushwa kwa kombora hilo, Korea Ksakzini ilisema kuwa kombora hilo la masafa marefu liliruika kwa dakika 47 na kufika urefu wa kilomita 3,724

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search