fURSA: Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa ujenzi bomba la mafuta ghafi...#share

JUMUIYA ya watoa Huduma wa Sekta ya Mafuta na Gesi (ATOGS) imewataka wadau kuchangamkia fursa zilizopo kabla na baada ya ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Uganda hadi Tanzania.

Ujenzi huo unaotarajiwa kuanza hivi karibuni utagharimu Dola za Marekani Biliioni 3.5 sawa na Sh. tirioni 8 za Kitanzania na unatarajia kuzalisha ajira kati ya 10,000 hadi 30000.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam  na Makamu Mwenyekiti wa (ATOGS) Abdulsamad Abdulrahim akizungumza na waandishi wa habari, amesema wanaunga mkono  Serikali ya Tanzania kwani watoa huduma waliopo Nchini wameonesha uwezo na utayari wa kutoa huduma nyingi katika mradi huo na kuchangamkia fursa zitokanazo na mradi.

Aidha ameteja fursa hizo zitokanazo na mradi huo wanazohamasishwa watoa huduma kuchangamukia  kuwa ni pamoja na ujenzi, ununuzi, uwezeshi, huduma za bima, kibenki, fedha, kisheria, ulinzi, chakula na dharura.

Amesema uongozi umeona umuhimu wa kuzipokea fursa na Makampuni yanayotoa huduma yamekwishajiunga na ATOGS na kuyaita makampuni mengine kujiunga ili yaweze kupata fursa zinazopatikana sasa na nyingine zinazoendelea kufunguka.
“Baada ya ufungunzi rasmi wa ujenzi wa bomba la mafuta na gesi utakaofanyika jumamosi wiki hii tarehe 5 mwezi 8 mwaka huu ambao mgeni rasmi ni Rais John Magufuli na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni katika kufanikisha ufunguzi wa mradi huo kwa ajili ya manufaa ya nchi mbili,”amesema Abdulirahim.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Juliana Palangyo amesema mradi unafursa kubwa na kuwaomba watoa huduma kupitia (ATOGS) kuungana katika kupata fursa inayotokana na mradi huo.

“Mradi huu una fusra nyingi kama ujenzi, biashara, utoaji huduma na chakula, zote hizi ni fusra zinazoitaji watu, pia ujenzi huu wa bomba la mafuta utaifikia mikoa 8 na wilaya zake ambayo ni Singida, Tanga, Shinyanga, Geita, Dodoma, Manyara, Kagera na Kahama ndani ya miezi 24,” amesema Palangyo.


Na Dalila Sharif.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search