sPORTS nEWS: Kapinga akabidhiwa mikoba ya Mgosi Simba, yeye apangiwa kazi nyingine..#share

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kikao cha kamati ya utendaji ya klabu ya Simba iliokutana hivi karibuni,imemteua Dr Cosmas Kapinga kuwa Meneja mpya wa Timu ya Simba


Dr kapinga anachukua nafasi ya Mussa Hassan Mgosi ambae amepangiwa majukumu mengine ndani ya klabu.
Kapinga ataanza kazi yake mpya,mara baada ya kikosi cha Simba kurejea nchini kutoka Afrika kusini,ambapo kwa sasa kipo katika maandalizi ya mwanzo wa msimu. 

Kwa upande wa Mgosi,sasa atakuwa kocha msaidizi na Meneja wa Timu ya vijana,sambamba na Nico Nyagawa ambae nae atakuwa kocha msaidizi wa kikosi hicho,huku pia akiwa mratibu,Kikosi hicho cha vijana kitaendelea kuwa chini ya kocha mkuu Nico kiondo. 

Katikati ya mwezi huu Mussa Mgosi atafanya mafunzo ya ukocha leseni C,ambayo yatampa fursa ya kuongeza ujuzi kwenye majukumu mapya ya ualimu ndani ya timu yetu.

Wakati huo huo,benchi la ufundi la Timu ya Simba,limeridhishwa na maandalizi yao huko Afrika kusini,huku pia likiridhishwa jinsi kikosi cha Simba kilivyocheza jana na Klabu ya Orlando Pirates.
Ingawa tumepoteza mchezo wetu wa jana,lakini tumeshaanza kupata mwelekeo wa kikosi,na katika siku chache zijazo,teyari tutakuwa tushapata kikosi cha kwanza"alisema Mwalimu Omog. 

Hapo kesho Timu hiyo itashuka kwenye dimba la Sturrock Park liliopo ndani ya Chuo kikuu cha Wits kilichopo Braamfontein Jijini Johannesburg kucheza mechi ya mwisho ya maandalizi nchini humo,dhidi ya Bidvest. 

Timu hiyo ndio mabingwa wa soka nchini Afrika kusini kwa sasa.
IMETOLEWA NA... HAJI MANARA
MKUU WA HABARI SIMBA SC

SIMBA NGUVU MOJA

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search