gOOD nEWS: WHC yashusha neema kwa watumishi Makao Makuu Dodoma...#share

KAMPUNI ya Watumishi Housing (WHC) imesema imeanza ujenzi wa nyumba 159 makao makuu ya nchi Dodoma katika kuunga mkono uamuzi wa serikali kuhamishia shughuli za kiserikali katika mkoa huo.


Hayo yamebeinishwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa WHC Fred Msemwa akizungumza na waandishi wa habari, amesema nia yao ni kuboresha maendeleo ya nchi.

“Watumishi Housing tumejipanga kuwajengea watumishi nyumba bora na za kisasa mkoani Dodoma katika eneo la Njedengwa, lililopo mkabala na eneo la Kisasa Dodoma,” amesema Msemwa.

Amesema kutokana na mpango wa serikali wa kuhamishia shughuli zake mkoani Dodoma kuja na fursa nyingi ikiwa moja wapo ni kuendeleza makazi ya watumishi, WHC ni jukumu lao la msingi kuhakikisha wanapata makazi bora na ya kisasa kwa bei nafuu.

Msemwa amebainisha kwamba kutokana na hali hiyo wameandaa ardhi ya ekari 55 za ardhi mkoani humo ambapo wanatarajia kujenga nyumba 500. Nyumba 159 zitajengwa katika awamu ya kwanza kwaajili ya watumishi watakao kuwa wakihamia Dodoma na wale wanaoishi Dodoma.

Ameweka wazi bei ya nyumba ya vyumba vitatu itaanzia sh. milioni 46 na amebainisha kuwa ujenzi wa nyumba hizo utachukua muda wa miezi nane kukamilika ambapo amesema zitakuwa za aina mbili yani zilizoisha kabisa (full finished) na zile zitakazokuwa zimeisha kwa asilimia 80, hivyo mtumishi atakuwa na fursa ya kuingia na kuishi huku akimalizia kwa kadri anavyopenda.

Aidha amesema bei za nyumba zilizokamilika itakuwa sh. milioni 59 pamoja na VAT na zile ambazo zimekamilika kwa asilimia 80 tayari kwa kutumika zitakuwa sh.milioni 46 pamoja na VAT huku zikilipwa kwa njia ya malipo endelevu wakati wa au wa mkopo wa bei nafuu toka kwa benki washirika na kurejesha ndani ya mwaka mmoja hadi miaka 25.

Kwa upende mwingine Mkurugenzi huyo amesema wamepokea mssada wa vifaa vya upimaji wa viwanja na miji ambavyo vitawasaidia katika kutoa huduma zote za makazi kuanzia uuzaji wa viwanja vilivyopimwa pamoja na nyumba zilizokamilika.

Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search