mAHAKAMANI kISUTU: Wema 'yamkuta mazito', Mkemia Mkuu adai mkojo wake una dawa za kulevya.....#shar
MAHAKAMA ya
Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imeelezwa kuwa, chembechembe za mkojo wa
msanii maarufu wa filamu nchini Wema Sepetu una dawa za kulevya.
Hayo
yamesemwa leo na Mkemia kutoka ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Elias Mulima
(40), ambaye ni shahidi wa kwanza katika kesi ya matumizi ya dawa za kulevya
inayomkabili Wema na wenzake wawili.
Akiongozwa na
Wakili wa Serikali, Constantine Kakula, Mulima amedai mbele ya Hakimu Mkazi
Mkuu , Thomas Simba kuwa Februari 8 mwaka huu, alipokea sampuli ya mkojo wa
Wema ambaye alifikishwa kwenye ofisi hizo akiwa na askari wawili, WP Mary na
Inspekta Willy.
Amedai kuwa
askari hao walieleza kuwa, walifika hapo kwa ajili ya kumpima mtuhumiwa Wema mkojo, ambapo kabla ya kumfanyia kipimo
alimsajili kisha akamakabidhi WP Mary kontena na kumchukua Wema hadi katika
choo maalumu kilichopo katika ofisi hizo kwa ajili ya mchakato huo hilo.
"Baada
ya kupata chembechembe za mkojo, nilifanya uchunguzi na kugundua kuwa, mkojo
wake ulikuwa na chembe chembe za bangi ambapo kitaalamu bangi inaonekana kwenye mkojo kwa siku 28",
alidai shahidi
Ameendelea
kueleza kuwa bangi inakemikali ambayo
inasababisha mtumiaji kuwa na ulevi ambao hauwezi kutibika kirahisi na mtumiaji
huharibika akili.
Amebainisha
kuwa kabla ya kupokea sampuli ya mkojo, alipokea bahasha kutoka jeshi la polisi
iliyopelekwa na Koplo Robert ambayo ndani yake alikuta msokoto na vipande
viwili vya bangi ambayo vilipelekwa pale kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa
kitaalamu.
Amedai baada
ya kuvipima vipande vile vilikuwa na uzito wa gramu 1.08 na baada ya kufanyia uchunguzi majani yale
yalioyesha kuwa na rangi ya zambarau
ambayo inaashiria kuwa yale majani ya mmea wa bangi pamoja na msokoto wa bangi. Aliandika
taarifa ya uchunguzi ambayo ilithibitishwa na mkemia mkuu.
Hata hivyo,
shahidi hiyo alipotaka kuwasilisha ripoti hizo kama kielelezo mahakamani wakili
wa utetezi, Peter Kibatala alipinga kielelezo hicho kupokelewa na kuidai kuwa
ripoti haikidhi vigezo vya sheria kwani mshitakiwa yoyote aliyeko chini ya
ulinzi kabla ya kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu ni lazima maombi yangepelekwa
kwanza mahakamani lakini polisi hawakufanya hivyo.
Naye wakili
Constantine alipinga vikali na kudai kuwa, hakuna kifungu kinachosema kuwa ni
lazima kupeleka maombi mahakamani kama mshtakiwa atakubalio kutii sheria.
Kufuatia
mabishano makali, Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 4, mwaka huu
itakapokuja kwa ajili ya uamuzi kama kielelezo hicho kipokelewe au la.
Na Mwandishi
Wetu
No comments:
Post a Comment