nEWS: Baada ya 'pedi mashuleni nchini Kenya' Rihanna nae apeleka baiskeli kwa wanafunzi Malawi.. #share.
Ikiwa ni mojawapo ya juhudi za Dunia kumkomboa mtoto wa kike kielimu,.. SuperStar katika tasnia ya muziki na urembo nchini Marekani, Mwanandada Rihanna, kupitia mojawapo ya ushirikiano kati ya wakfu wa Rihanna & Clara Lionel Fountaion kupitia kampuni Ofo kutoka China, imeanza kutoa ufadhili wa baiskeli kwa watoto wa kike Nchini Malawi.
Kampeni hiyo maarufu kwa jina 1km Action, itatoa ufadhili huo ili kuwasaidia mamia ya wasichana kuhudhuria shule za upili nchini malawi.
Wale watakaofuzu kupata ufadhili huo watapewa baiskeli ili kuhakikisha wanakwenda shule na kukamilisha masomo yao ya upili ambapo kwa sasa inakisiwa ni chini asilimia 10 ya wanafunzi hukamilisha masomo yao Nchini humo.. sababu ya usafiri ikitajwa miongoni mwa vikwazo vikuu.
''Nina furaha sana kuhusu ushirikiano na wakfu wa Clara na Ofo kwa sababu utawasaidia wasichana wengi dunini kupata elimu bora, pia watamaliza shule wakiwa salama zaidi kwani itawapunguzia mwendo kutoka majumbani mwao hadi mashuleni'' alisema Rihanna akielezea furaha yake juu ya mradi huo..
![]() |
Rihanna aki-show-off pamoja na mwanawe na mpenzi wake.. |
Wale watakaofuzu kupata ufadhili huo watapewa baiskeli ili kuhakikisha wanakwenda shule na kukamilisha masomo yao ya upili ambapo kwa sasa inakisiwa ni chini asilimia 10 ya wanafunzi hukamilisha masomo yao Nchini humo.. sababu ya usafiri ikitajwa miongoni mwa vikwazo vikuu.
''Nina furaha sana kuhusu ushirikiano na wakfu wa Clara na Ofo kwa sababu utawasaidia wasichana wengi dunini kupata elimu bora, pia watamaliza shule wakiwa salama zaidi kwani itawapunguzia mwendo kutoka majumbani mwao hadi mashuleni'' alisema Rihanna akielezea furaha yake juu ya mradi huo..
No comments:
Post a Comment