nEWS:JPM aipoka JKT ardhi na kurudisha mikononi mwa wananchi Tanga...#share


RAIS Magufuli amerudisha kwa wananchi eneo la ardhi ambalo Jeshi la Kujenga Taifa (Mgambo JKT) Mkata, Wilayani Handeni Mkoani Tanga, lilishindwa kuliendeleza kwa muda wa miaka saba.


Amekifia hatua hiyo leo wakati akisalimiana na wananchi wa eneo hilo akiwa safarini, baada ya kiongozi wa JKT kukiri kuwa walishindwa kuliendeleza katika kipindi hicho tangu walipopewa na kijiji ili kujenga kiwanda.

Badala yake Rais Magufuli ameagiza kiwanda hicho kijengwe ndani ya eneo la JKT ambalo tayari lina miundombinu ya maji na umeme.

“Eneo la mgambo JKT niameambiwa haliendelezwa katika kipindi cha miaka saba, warudishiwe wananchi waliendeleze kwa kazi za kilimo, kiwanda mkajenge hapohapo, ardhi ya wananchi muirudishe,”alisisitiza.

Aidha, Rais Magufuli amewaonya vijana akiwataka kuacha kutumika kwa kutegemea fedha za bure, badala yake wafanye kazi zikiwemo za kilimo ili kujipatia maendeleo.

Kuhusu suala la afya, Rais Magufuli amesema Serikali imetenga Sh. milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya huku akiwataka wananchi kushirikiana na tume itakayoundwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Njia Wazee na Watoto kuchunguza ubadhilifu wa sh. milioni 500 zilizotolewa awali kwa ajili hiyo.

Magufuli amesema lazima hospitali ya wilaya ijengwe kwa kuwa hawezi kukubali eneo la kutoka Mkata hadi Chalinze kutokuwa na hospitali ya wilaya, kwani kuwepo kwake watu wanufaika hawatakuwa wananchi wa eneo hilo tu.

Kuhusu maji, Rais amesema mradi kutoka Mto Wami unaotarajiwa kugharimu sh. trilioni 4, hadi sasa serikali imeshatoa nusu ya kiasi hicho na tayari mabomba yameshatandazwa ilikuondoa changamoto ya kukosa nishati hiyo kwa wananchi Mkata.

Aidha, amewashukuru wananchi wa eneo hilo kwa kumpa kura huku akiahidi kuwahudumia kwa kuhakikisha anaondoa kero zao.

Rais Magufuli yupo safarini ambapo Agosti 5 atakutana na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kwa ajili ya kuweka jiwi la msingi la mradi wa bomba la kusafirisha mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.









Na Mwandishi Wetu



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search