sPORTS nEWS: CUF yatokwa povu Zanzibar kuvuliwa uanachama CAF, yataka hatua zichukuliwe....#share

CHAMA cha Wnanchi CUF kimelaani na kupinga vikali hatua ya Chama cha Mpira Barani Afrika (CAF) kuwavua uanachama kwani kitendo hicho wamekifananisha na Zanzibar kuvuliwa nguo.


Kauli hiyo imetolewa leo mjini Zanzibar na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Nassoro Ahmed Mazrui akizungumza na waandishi wa habari, alisema si kitendo cha kuvumilika hata kidogo.

“Mbali ya kukilaani, bali pia ni haki yetu kukipinga. Na zaidi ya kukilaani na kukipinga, CUF inaona tuna wajibu wa kudai kupata maelezo ya kutosha, kutoa taarifa/taaluma ya kutosha kwa CAF na kukikatia rufani kadiri ya Kanuni zinazohusika zilivyo ili tukisemee, tukisimamie na tukitafutie suluhu,” amesema Mazrui.

Aidha amebainisha kwamba walitegemea viongozi wa Zanzibar na Muungano wangelilisemea jambo hilo kwa nguvu inayopaswa kusemewa, lakini hawajaona hatua thabiti za kuukabili msiba huo kwa Zanzibar.
Mazrui alieleza wameshindwa kusikia sauti ya kuunguruma kuzungumzia tukio hilo, ambalo limewarudisha nyuma baada ya kuonekana wamepiga hatua moja kubwa na ya maana kwa nchi yeo.

Amesema kuwa pamoja na kuvuliwa huko kuwa ni kwa mujibu washeria lakini wanaona kwamba waanayo nafasi ya kuielezea CAF kuwa haiko sahihi katika uamuzi wake kwa hoja ambazo imezitoa.

Ameeleza, CAF ilichokifanyia maamuzi ni kukosekana kipengele cha kuchukua hatua ndani ya mipaka ya sheria kwa kesi kama ya Zanzibar ambayo haifanani na nyengine yoyote hapa Afrika kwa waliokubaliwa wanachama wa CAF.

Amefafanua kwamba CAF imetoa hoja kuu mbili zilizopelekea kuinyang’anya Zanzibar kiti chake katika chombo hicho. Moja, ni kwamba haiwezi kutoa nafasi mbili kwa nchi moja kuwakilishwa na pili, ni kuwa kigezo cha uanachama ni kuwa nchi hiyo ni mwanachama wa UN. Hoja ambazo zote wamedai kwamba  dhaifu.

Mazrui amesema CUF inaamini kuwa ni vyema hili likasimamiwa kwa makini zaidi katika kuelekea kukata rufaa au kupinga uamuzi wa CAF wa kuitoa Zanzibar baada ya kupitishwa na Mkutano Mkuu na tuna hoja zifuatazo:

Amesema kutokana na hali hiyo wametaka baadhi ya haya yafanyike, wamewataka wahusika kutoka Zanzibar wasilifanyie ajizi jambo hilo na lifuatiliwe kwa utaalamu na umakini.

Aidha ametaka wahusika waiarifu CAF kuwa kuwaambia wawakilishwe na TFF katika mazingira yaliopo sasa ni kunakaribisha ukoloni mamboleo, kwa sababu kikatiba na kisheria ni suala ambalo haliwezekani.

Amesema njia peke ya kutoka katika hilo ni kuishawishi CAF iunde Tume Maalum kulifuatilia suala hili kwa kina na undani unaostahiki.

Ameeleza iwapo jambo hilo ni kwa maslahi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, CUF imetaka kuona unakuwepo mkazo wa hali ya juu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na kuhusishwa kikamilifu Wizara ya Mambo ya Nje ambayo inapaswa kusimamia maslahi ya Tanganyika na Zanzibar kwa usawa.


Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search