Bad News: Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akionyeshwa Nguo za Lissu zilizotapakaa damu..#share
MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe amesema Mbunge wa
Singida Mashariki, Tundu Lissu amepigwa risasi leo Alhamisi nyumbani kwake na
kwamba hali yake ni mbaya.
Lissu, ambaye ni mwanasheria mkuu wa Chadema kwa sasa
amepelekwa chumba cha upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma.
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, wabunge na viongozi
wengine wa ulinzi wa Bunge wamefika katika hospitali hiyo kujua kinachoendelea.
Baadhi ya ndugu na wagonjwa wamefurika katika chumba cha
upasuaji cha hospitali ya mkoa wakitafakari, huku wengine wakilia.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Charles Kihologwe amewataka
watu hao kukaa mbali na chumba cha upasuaji lakini wengi wanakataa wakisema
hawamwamini mtu yeyote.
Asubuhi, Lissu alihudhuria kikao cha Bunge na aliomba
mwongozo wa Naibu Spika akihoji kuhusu taarifa za kamati zilizoundwa na Spika
wa Bunge, Job Ndugai kutathmini mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na
udhibiti wa madini ya Tanzanite na almasi kuwasilishwa kwa Waziri Mkuu badala
ya kujadiliwa na Bunge kwanza.




No comments:
Post a Comment