NEC yateu Mbunge mwingine CUF kujaza ya aliyefariki....Pia yateua madiwani 3 viti maalumu..#share
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemteua Rehema Migira kuwa
Mbunge wa viti maalum kupitia Chama Cha (CUF) kujaza nafasi ya Mbunge mteule Hindu
Mwenda aliyefariki Septemba 1 mwaka huu.
Akizungumza jijini Dar es Salam leo Mkurugenzi Mkuu wa NEC Kailima Ramadhan, amesema wamefanya
uteuzi huo baada ya kupata taarifa kutoka wa spika wa bunge, Job Ndugai kuwepo
kwa nafasi moja ya ubunge kufutia kifo cha mbunge huyo mteule aliyefariki kabla
ya kuapishwa.
"NEC imemteua ndugu Rehema Juma Migira kuwa mbunge wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupata taarifa kutoka wa spika ambaye
alitutaarifu kuwepo kwa nafasi moja ya wazi ya viti maalumu kupitia chama cha
CUF baada ya aliyeteuliwa kuwa mbunge wa viti maalum CUF kufariki dunia"
amesema Ramadhan.
Aidha ameendelea kusema kuwa tume hiyo imefanya uteuzi pia wa
madiwani wa viti maalum watatu kujaza nafasi zilizo wazi katika halimashauri za
Tanzania Bara.
Ramadhan ametaja madiwani hao kuwa ni pamoja na Jane Chungwa ambaye anakuwa diwani wa viti
maalum halmshauri ya Itigi Singida, Osana
Mwinyi anakuwa diwani wa viti maalum halmshauri ya Bahi Dodoma wote Chama cha
Mapinduzi (CCM).
Mwingine ni Pili Mfaume kutoka Chama cha Wananchi CUF anayekuwa Diwani wa Viti Maalum Halmshauri ya Temeke,
uteuzi huo wa madiwani umefanyika baada ya tume kupata taarifa ya kuwepo kwa
nafasi hizo wazi kutoka kwa waziri mwenye dhamana ya serikali za mitaa.
Na Abraham Ntambara




No comments:
Post a Comment