Habari Njema: Benki ya kilimo yaongeza kiasi cha mikopo kutoka Sh bilioni 1 hadi sh bilioni 8.917

BENKI ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB)imesema imeongeza kiasi cha mikopo kwa 

wakulima wadogo wadogo kutoka Sh bilioni 1.0 hadi Sh bilioni 8.917 huku ikibainisha 

kukopesha wakulima 2,610 lengo likiwa kuwanufaisha na kuwakawamua kiuchumi.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa 

TADB,Francis Assenga wakati akizungumza na wanahabari kuhusu benki hiyo kutimiza 

miaka miwili ya utoaji huduma na mikakati yake ya kujitanua kupitia kongani.

Amebainisha kuwa tangu benki hiyo ianzishwe imekuwa ikipiga hatua katika 

kuwahudumia wakulima ikiwemo kuwawezesha kupata mikopo inayowasaidia kufanya kilimo 

cha kisasa na chenye tija huku akisisitiza benki hiyo imejzatiti kuwafikia wakulima wote

''Benki inaendelea kufanya uchambuzi wa miradi 17 yenye thamani ya zaid8i ya sh 

bilioni 35.473 pia tumeweza kukopesha kutoka vikundi nane hadi vikundi 21, taasisi 

moja ya umma na kampuni moja ya maziwa,'' alisema Assenga.

Ameongeza kuwa TADB imeweza kuvijengea uwezo vikundi 672 vya wakuluima wadogo 

wadogo vyenye jumla ya wanachama 91,684 kutoka vikundi 336 vilivyokuwa vinajumuisha 

wakulima ha9o 44,000 katika mikoa ya Iringa, Morogoro na Tanga.

Amefafanua kuwa benki hiyo imewaunganisha wakulima wadogo 2,328 na wanunuzi kwenye 

mnyororo wa thamani wa mazao ya mahindi,mpunga, mbogamboga na miwa.

Aidha, amesema TADB imeweza kupata fedha zaidi za kukopesha kutoka Serikalini kiasi 

cha Sh bilioni 209.5 huku akibainisha nusu ya fedha hizo zimeshapatikana kutoka 

Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Pia amesema wataongeza wigo wa utoaji huduma kutoka mikoa sita kwenda kanda nane 

kwa uratibu wa kongani ya idadi ya kipaumbele toka mikoa 14 hadi 20 kulingana na 

vipaumbele vya mikoa.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search