JPM amewataka viongozi wote waliotajwa katika ripoti za Bunge ya Madini ya Almasi na Tanzanite kujitumbua kupisha uchunguzi..share
RAIS John Magufuli
amewataka viongozi mbalimbali wa serikali ambao wametajwa kwenye ripoti za
bunge ya madini ya Almasi na Tanzanite waachie nafasi zao ili vyombo vya
usalama viweze kufanya kazi yake vizuri ya kuwachunguza.
Rais Magufuli amesema
hayo leo wakati akikabidhiwa ripoti
hizo Ikulu jijini Dar es Salaam na Waziri
Mkuu Kassim
Majaliwa na kusema amesikia baadhi ya viongozi
mbalimbali wengine
ambao amewateuwa yeye kuwa wameusishwa kwenye wizi huo hivyo amewataka wapishe.
"Wako watu wametajwa tajwa, na wengine mimi ndio
nilihusika kuwateua sasa ukishatajwa tajwa, naagiza vyombo vya ulinzi na
usalama vifuatilie hili tena kwa haraka.
" Wale ambao wametajwa tajwa kwenye ripoti hii ambao ni
wateule wangu, ili vyombo vya usalama viweze kufanya kazi yake vizuri, ni
matumaini yangu watakaa pembeni" alisema Rais
Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipitia Taarifa ya Kamati Maalum ya Bunge ya Kuchunguza Madini ya Almasi na Tanzanite mara baada ya kukabidhiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwenye hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam
Katika ripoti hiyo
ambayo iliwasilishwa jana mjini Dodoma na leo kukabidhiwa kwa Rais Magufuli na
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa iliweza kuwataja baadhi ya viongozi wa serikali
ikiwepo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) Mh. George Simbachawene, Waziri wa zamani wa Nishati na Madini na
Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja pamoja na aliyekuwa Waziri wa Nishati na
Madini, Profesa Sospeter Muhongo.






No comments:
Post a Comment