Sports News: Mahakamani Kisutu leo Malinzi na wenzake kesi yao imeahirishwa...Warudishwa rumande hadi ...#share
ALIYEKUWA Rais Wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchin (TFF) Jamal Malinzi na wenzake wawili, leo wamefika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kusikiliza kesi yao inayowakabili.
Malinzi na wenzake wanatuhumiwa kwa makosa mbalimbali yakiwemo ya matumizi mabaya ya madaraka waliyokuwa nayo katika uongozi wao
pamoja na kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya TFF.
Aidha kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 21 mwaka huu baada
ya hakimu anayesikiliza shauri hilo kutokuwepo kutokana na kuwa na dharura.
Hayo yamebainishwa na Wakili wa Serikali, Faraj Ngokah mbele
ya mahakama na kusema upelelezi wa kesi hiyo hujakamalika
huku ikielezwa kuwa Hakimu anayesikiliza shauri hilo, Wilbard Mashauri amepatwa
na dharura.
Kutokana na hayo, Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa
ameahirisha kesi hiyo hadi Septemba 21 mwaka huu itakapotajwa kwa mara
nyingine.
Na Mwandishi Wetu




No comments:
Post a Comment