sPORTS nEWS: Sanga,Yahya kuwania kiti Bodi ya Ligi.....#share
KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imepitisha majina ya wagombea wafuatao kuwania uongozi katika nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Kamati ya Uongozi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) ambapo Kaimu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga atachuana na Ahmad Yahya atayetetea nafasi ya uenyekiti.
Clement Sanga
Sanga na Yahya wanatokea katika klabu za Ligi Kuu ya
Tanzania, za Yanga ambapo Sanga anakaimu nafasi ya uenyekiti baada ya Yusuf
Manji kujiuzulu kwa sabau za kiafya.
Kwa wa mujibu wa taarifa ya TFF iliotolewa kwa vyombo vya
habari leo, majina hayo yamepitishwa mara baada ya kuwafanyia usaili Jumapili
Septemba 3, mwaka huu kwenye Ukumbi wa TFF, Dar es Salaam. Uchaguzi utafanyika
Oktoba 15, mwaka huu.
Kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi inayotokana na kanuni za
uchaguzi za TFF, majina hayo yanapaswa kutangazwa sasa.
Ahmad Yahya (kushoto) kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura
Wanaowania nafasi ya ujumbe ni Hamisi Madaki na Ramadhani
Mahano wanatokea Klabu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Pia yumo Almasi Kasongo anayewania nafasi hiyo kupitia
Klabu za Ligi Daraja la Kwanza huku Edgar Chibura akiwania nafasi ya ujumbe
kupitia Klabu za Ligi Daraja la Pili wakati huo huo,
Wakati huohuo, TFF, imeagiza Makatibu wa Vyama vya Mikoa kutuma haraka
majina ya timu mabingwa wa mikoa wa soka la wanawake wa msimu wa 2016/17.
Viongozi wa mikoa wamekumbushwa kutuma timu ili kufanya
maandilizi ya haraka ya Ligi Ndogo itakayofanyika Septemba 22 hadi 29, mwaka
huu.
Ligi Hiyo ndogo inachezwa kutafuta timu mbili zitakazopanda
daraja kucheza Ligi Kuu soka ya wanawake msimu wa 2017/2018.
Huu ni msimu wa pili wa ligi ya wanawake kwani msimu
uliopita, timu shiriki zilikuwa 12 na Mlandizi Queens ya Pwani iliibuka bingwa
wa kwanza katika historia ya soka hapa nchini.
Mara baada ya kumalizika kwa Ligi Ndogo, TFF itaanza taratibu
za kupanga kuanza kwa Ligi Kuu kwani wakati huo tayari tutafahamu timu ambazo
zimepanda. Ligi Ndogo haitahusisha timu ambazo zimecheza Ligi Kuu msimu wa
2016/17.
Na Mwandishi Wetu





No comments:
Post a Comment