sPORTS nEWS: TFF yaweka Sheria za Soka Pembeni...Busara yatumika kumtoa Buswita wa Yanga Kifungoni...#share
SAKATA la kiungo mshambuliaji Pius Buswita kufungiwa,
limefika mwisho baada ya kupatiwa ufumbuzi na mchezajii huyo atakuwa na nafasi
ya kuichezea Yanga katika msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Sakata hilo lilitokana na mchezaji huyo kusaini mikataba miwili tofauti ya
kuzitumikia klabu za Simba na Yanga jambo ambalo lilisababisha kufungiwa mwaka
mmoja na kamati ya katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji kwa kuwa ni kinyume na
sheria mchezaji mmoja kusaini sehemu mbili tofauti.
Akizungumzia suala hilo leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti
wa Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji, Elias Mwanjala amesema klabu
hizo mbili zimefanya mazungumzo nakuafikiana juu ya mchezji huyo.
Mwanjala amesema kuwa baada ya Simba na Yanga kukubaliana juu
ya mchezaji huyo ili atoke kifungoni, Yanga itatakiwa kuilipa Simba shilingi
milioni 10 ambazo Buswita alizichukua aliposaini Simba.
Amebainishwa kuwa Buswita atakuwa tayari kuitumikia klabu
yake Mpya ya Yanga itakapokuwa imekamilisha kuilipa Simba kiasi hicho cha
Fedha.
Na Mwandishi Wetu




No comments:
Post a Comment