Tucta yajitosa kupigwa risasi kwa Lissu.. Yasema alifanyiwa kitendo cha Kihuni....#share

KATIBU Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Dk.Yahya Msigwa amelaani kitendo cha kihuni cha kupigwa kwa risasi mchana kweupe Mbunge wa Singinda Mashariki, Tundu Lisu.

Matukio mengine ambayo hayatakiwi kufumbiwa macho ni pamoja na utekaji raia, utekeji watoto wadogo na mauaji kwa baadhi yao, mauaji ya kijambazi ya watu wasio na hatia, Kibiti, Mkuranga na Kilwa.

Dk. Yahya ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.

 Amesema Tanzania tumezoea kuwa kisiwa cha amani na kutofautiana kwa hoja na fikra na kujijengea utamaduni wa kupinga bila kupigana  kuamini kuwa hoja inajibiwa kwa hoja.

"Kitendo hicho kimetushtua raia wa Tanzania na Ulimwanguni kote, hivyo vyombo vya dola vinapaswa kutekeleza wajibu wao," alisema.

Ameeleza vitendo hivyo visipokemewa na kulaaniwa yatatuchafulia nchi taswira nzuri tuliyojijengea kwenye uso wa kimataifa,hivyo TUCTA wamelaani matendo yote maovu.

Ameongeza kwa kuiomba serikali kutumia vyombo vyake vya dola kufanya jitihada ya kuwajua wahalifu ili kukomesha matukio hayo ya kihuni kutokea.

Aidha, amesema ili huduma au uzalishaji ufanyika katika jamii msingi wake ni amani, iwapo amani itatoweka watu hawawezi kwenda kanisani wala Misikitini kuabudu.

Amesema dalili zilizojitokeza zinaonesha amani yetu ipo hatarini kutoweka iwapo hatua za makusudi hazitachukuliwa kwa ajili ya  kudhibiti.

"Tusikubali lulu ya Tanzania kupotea, hivyo tusikubali jambo lolote kutokea kuharibu amani yetu, tuitunze na kuilinda," amesema.

Na Mwandishi Wetu


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search