Zitto, Kubenea wamjeruhi Spika Ndugai...Awageukia kama Mbogo na kuwapeleka kwa pilato..#share
SPIKA wa Bunge Job Ndugai amamtaka Mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Saed Kubenea kufika kesho mbele ya Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama ili kuhojiwa kwa kumtuhumu kuwa spika ni muongo.
Spika Ndugai amesema kuwa Kubenea amemtuhumu kwamba amedanganya idadi ya risasi alizopigwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) na Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyia (TLS) Tundu Lissu.
Katika hatua nyingine Ndugai ameagiza Kubenea na Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya Chamka cha ACT- Wazalendo Zitto Kabwe kupelekwa katika Kamati ya Bunge ya Maadili na Madaraka kwa tuhuma mbili tofauti zinazowakabili.
Tuma hizo ni kwamba Zitto anatuhumiwa kwa kutamka kuwa Bunge limewekwa mfukoni na muhimili fulani, wakati Kubenea ni kwa kumtuhumu Spika kusema uongo wa idadi ya risasi alizopigwa Lissu.
Na Mwandishi Wetu.





No comments:
Post a Comment