Aliyekamatwa na mamilioni uwanja wa ndege apandishwa kizimbani...soma habari kamili na matukio360..#share


Na Abdulrahim Sadiki, Dar es salaam
Siku chache baada ya Rais John Magufuli kubainisha kukamatwa kwa kiasi kikubwa cha fedha katika Uwanja wa  Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) aliyekamatwa na fedha hizo amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.


Mshtakiwa huyo ni raia wa Uganda, ambaye ni Kalani wa Kampuni ya Ulinzi ya SGA, Winfred  Businge (33).

Busige amefikishwa mahakamani akikabiliwa na kosa la kushindwa kuelezea kwa mamlaka ya forodha fedha alizokamatwa nazo Airpot ambazo ni USD Milioni moja takribani bilioni  mbili.

Wakili wa serikali mwandamizi, Awamu Mbagwa amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa mshtakiwa anakabiliwa na kosa moja.

Amedai kuwa kosa hilo amelitenda kinyume na kanuni za sheria za utakatishaji fedha, ambayo haimnyimi mshtakiwa dhamana.

Wakili Mbagwa amedai kuwa Businge ametenda kosa hilo Disemba 11,2017 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Inadaiwa akiwa ndani ya jiji la Dar es Salaam alikutwa ameingia nchini akiwa na USD Milioni 1 (zaidi ya Sh.Bil 2)ambazo alishindwa kuzitolea maelezo kwa wakala wa forodha.

Baada ya kusomewa kosa hilo, mshtakiwa alikana kosa, ambapo wakili Mbagwa alieleza kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na anaomba tarehe kwa ajili ya kumsomea mshtakiwa maelezo ya awali.

Hata hivyo, wakili wa utetezi Emmanuel Safari alimuombea dhamana mteja wake.

Hakimu Shaidi alimuachia mshtakiwa huyo kwa masharti ya dhamana ya mdhamini mmoja bila kusaini bondi.


Hakimu Shaidi alisema amemuachia kwa dhamana bila bondi kwa sababu fedha zilizokamatwa zitakuwa kama dhamana yake.Kesi imeahirishwa hadi January 18,2018.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search