Makamo wa rais Zanzibar 'awalilia' wafanyabiashara...soma habari kamili na matukio360..#share


Na Mwajuma Juma, Zanzibar

MAKAMO wa pili wa rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi amesema wakati umefika kwa wafanyabiashara wakubwa Zanzibar kuwekeza katika bidhaa za kiswahili hususan katika uchapishaji wa vitabu vya kiswahili pamoja na kujenga maduka makubwa ya kuuzia bidhaa hizo.
Makamo wa pili wa rais Zanzibar, Balozi Seif Idd

Ametoa wito huo leo katika ufungaji wa kongamano la kiswahili lililofanyika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Amesema  hatua hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa ongezeko la   utungaji wa vitabu vya kiswahili na usomaji.

Amesema  pamoja na kuwa Zanzibar ina watunzi wengi wa vitabu vya kiswahili lakini imekuwa tabu kuvipata vitabu  kutokana na kuwa hakuna  utaratibu mzuri wa upatikanaji wake.

“Kiswahili ni bidhaa inayouzika, wakati umewadia kwa wafanyabiashara wetu wakubwa kuwekeza katika bidhaa hii katika uchapishaji wa vitabu vya kiswhaili, leo hii hapa Zanzibar ukitaka vitabu vya waandishi wetu mashuhuri kama Profesa Said Ahmed , Shafi Adam Shafi, Bwana Musa na ndugu yangu Mohammed Seif Khatib huvipati”, amesema Balozi Seif.



Makamo huyo wa rais amesema ni wakati muafaka sasa kufikiria kuandaa maonesho ya kimtaiafa ya vitabu vya kiswahili katika ukanda wa Afrika Mashariki yatakayokuwa kila baada ya miaka miwili au zaidi.

Amesema maonesho hayo pia yatasaidia kuongeza kasi ya uchapishaji na usomaji vitabu.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search