CCM yamkabidhi kadi aliyekuwa mbunge wa Kinondoni...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu
CHAMA cha Mapinduzi(CCM) leo kinatarajia kumpokea rasmi aliyekuwa mbunge wa Kinondoni(CUF), Maulid Mtulia.
Aliyekuwa mbunge wa Kinondoni(CUF), Maulid Mtulia

Hatua hiyo inafuatia Mtulia juzi kujiuzulu nafasi yake hiyo pamoja na kujivua uanachama wa CUF.

Taarifa za ndani iliyozifikia matukio360 mapema hii leo zinadai Mtulia atakabidhiwa kadi ya CCM katika ofisi za  chama hicho zilizopo Kijitonyama kwa Alimau jijini Dar es Salaam.

" Leo(Jumatatu) majira ya mchana, CCM inamkabidhi rasmi kadi Mtulia aliyekuwa mbunge wa Kinondoni, tukio litafanyika katika ofisi ya chama Kijitonyama kwa Alimaua,’’ kilisema chanzo  chetu cha kuaminika ndani ya CCM

Chama cha CUF kimebariki uamuzi wa Mtulia na kimemtakia kila la kheli.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search