Marekani, Korea Kaskazini wajibizana...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
MSHAURI wa masuala ya usalama wa Ikulu ya White House nchini Marekani, HR McMaster amesema  Marekani iko mbioni kukabiliana na tishio kutoka Korea Kaskazini

Kombora la Hwasong-15 lililopaa  na lenye uwezo zaidi ya makombora mengine ya Korea Kaskazini lililojaribiwa hivi karibuni

Nayo Korea Kaskazini imedai Marekani ndio inayochochea msunguano huo utakaosababisha vita .

Hata hivyo HR McMaster amesema uwezekano wa kutokea vita unaongezeka kila siku lakini vita sio suluhu pekee, aliuambia mkutano wa ulinzi.

Matamshi yake yanakuja siku tatu baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio lake la kwanza la kombora la masafa marefu katika miezi miwili kinyume na vikwazo vya Umoja wa Mataifa.

Kombora hilo lilipaa mbali  zaidi ya  makombora mengine ambayo yalijaribiwa awali kabla ya kuanguka katika bahari ya Japan.
HR McMaster ameitaka China kuiwekea vikwazo vya mafuta taifa hilo ili kufanya kuwa vigumu kwa Pyongyang kujaza mafuta makombora yanayofanyiwa majaribio.

Hata hivyo ikijibu mapigo Korea Kaskazini imeishutumu Marekani kwa kuchochea vita.
Imetaja zoezi la pamoja la kijeshi kati ya Korea kusini na Marekani kuwa la uchochezi na kwamba linaweza kusababisha vita.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search