Charles Kimei 'bye bye' CRDB......soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei ametangaza kuwa hataongeza mkataba wake mara utakapofikia ukomo Mei 31, 2019.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, amesema amekuwa katika nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka 20 hivyo umekaribia wakati wake wa kumwachia mtu mwingine.

“Nimekuwa mkurugenzi mtendaji wa Benki ya CRDB kwa takribani miaka 20 sasa, hivyo wakati umekaribia kwangu mimi kumwachia mtu mwingine nafasi hii na mimi kuendelea kufanya majukumu mengine,” amesema Dk. Kimei.

Ameongeza “Kufuatia sera ya kurithisha nafasi ya mkurugenzi mtendaji wa Benki yetu hii, ifikapo Januari 2018, Bodi ya Benki inalazimika kuanza mchakato kwa ajili ya kujaza nafasi hii muhimu kwa mustakabali wa Benki ya CRDB,”

Dk. Kimei amesema mchakato wa kumtafuta Mkurugenzi Mtendaji mpya umekwisha anza na sababu ya kuanza mapema ni ili kuhakikisha zoezi linafanyika kwa uangalifu na kutoa muda wa kutosha wa kupata uidhinisho wa mamlaka husika kwa mtu atakayechaguliwa kushika nafasi hiyo.

Amewahakikishia wateja wa benki hiyo na watanzania kwamba benki ni salama na itaendelea kuwa salama.

“Tunatangaza hili mapema ili kuepusha dhana au hisia ya kwamba mkurugenzi mkuu anaondoka kwa vile kuna tatizo, au benki inaweza kuyumba. Niko kwa takribani miezi 18 na mioyo ya wateja ibaki na amani,” amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search