Yanga, Simba, Azam kutua Zanzibar Januari mosi....soma habari kamili na matukio360...#share

 Na Mwajuma Juma, Zanzibar
MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi inatarajiwa kuanza rasmi kesho ambapo jumla ya michezo mitatu itachezwa huku Simba, Yanga na Azam zikitarajiwa kuwasili Januari Mosi, 2018.
 Kikosi cha timu ya soka ya Yanga

Michuano hiyo ambayo itachezwa katika uwanja wa Aman mjini Unguja, itachezwa kuanzia majira ya saa 8:00 mchana na ufunguzi rasmi utakuwa majira ya saa 10:00 za jioni.

Katibu msaidizi  kamati ya kusimamia mashindano hayo Khamis Shaali amesema  saa 8:00 kutakuwa na mchezo kati ya Mlandege na JKU, saa 10:00 Jamhuri itapambana na Mwenge huku majira ya saa 2:00 usiku kutakuwa na mchezo utakaowakutanisha Zimamoto na Taifa ya Jang’ombe.

Amesema maandalizi  ya michuano hiyo imekamilika na timu ya Mwenge kutoka Pemba iliwasili jana na Jamhuri inawasili leo.

Amesema  timu kutoka Pemba zinajitegemea  huku timu kutoka Tanzania Bara ambazo ni Yanga, Azam, Singida United na Simba zitapangiwa Hoteli.

“Tumeenda kuweka 'booking' katika hoteli mbili moja ni Zanzibar Ocean View na nyingine ni Maruhubi Beach Villa lakini bado hatujalipa  fedha za mwanzo  kwa hiyo hatujajua ni ipi kati ya hiyo tutaziweka timu hizo,”  amesema.

Jumla ya timu 11zinatarajiwa kushiriki michuano hiyo ambapo kwa Zanzibar timu zinazoshiriki ni JKU, Zimamoto, Taifa ya Jang’ombe, Mlandege, Jamhuri  na Mwenge na kwa Tanzania Bara ni Simba, Yanga, Azam FC na  Singida United na kwa nje ya Tanzania ni  URA ya Uganda

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search