Dk Mndolwa mwenyekiti mpya jumuiya ya wazazi CCM...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mwandishi wetu, Dodoma
MKUTANO mkuu wa jumuiya ya wazazi wa CCM, leo wamemchagua Dk  Edmund Bernad Mndolwa kuwa mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo.


Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya wazazi CCM, Dk. Edmund Mndolwa

Dk Mndolwa ambaye aliwahi kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa, wilaya ya Korogwe vijijini mkoani Tanga, amepata kura 554, makamu wake ni  Haidar Haji Abdalah aliyepata kura 462.

Wajumbe wa NEC kutoka Tanzania bara  ni Edward Sokoine amepata 607, Mohammed Nasoro Ngongite amepata kura384, Paul Herman Kirigini amepata 343.
Wajumbe wa NEC  kutoka Zanzibar  ni Amina Ali Mohammed amepata kura 498, Juma seleman Kimei amepata 451, wajumbe wa baraza wa jumuiya hiyo kutoka bara  ni Lulu Mabasi Mtemvu ,Stephen Maji Marefu na Sufi kasim Sudi.
Baraza kutoka Zanzibar ni  Ali issa Ali, Christina Joram Anthony, Habiba Ali Mohamedi.
Mwakilishi umoja wa wanawake ni Bainaga Kassian Nuru  na wa Uvccm ni Omary Ajili Kalolo

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search