NEC yaituliza Ukawa....soma habari kamili na matukio360...#share


Na mwandishi wetu, Dar es Salaam
TUME ya taifa ya uchaguzi(NEC) imewataka wadau na vyama vya siasa kufuata utaratibu wa kisheria na kwamba ratiba ya uchaguzi wa marudio wa ubunge na udiwani wa Januari 13, 2018 haitobadilika.

Pia imesema hata ikitokea mgombea akawa ni mmoja, atapigiwa kura na kutangazwa kuwa mshindi.
Mkurugenzi wa uchaguzi Nec,Ramadhani Kailima

Msimamo huo umetolewa  leo jijini Dar es salaam na mkurugenzi wa uchaguzi NEC, Kailima Ramadhani alipokuwa akizungumza na matukio360.

‘’Nec inafanya shughuli zake kwa kuzingatia na kufuata sheria hivyo wadau na vyama vya siasa ni lazima navyo vifuate sheria katika kufanya maamuzi,’’ amesema Kailima

Amesema uamuzi wa vyama vinavyounda Ukawa kutaka uchaguzi uahirishwe haitowezekana na zaidi wafuate taratibu za kisheria ili kufanikisha hilo.

 Jana mwenyekiti taifa wa Chadema, Freeman Mbowe kwa niaba ya Ukawa alitaka uchaguzi uahirishwe akida mazingira hayako sawa na kwamba serikali na Nec ikikata kufanya hivyo, vyama vinavyounda umoja huo havitoshiriki uchaguzi huo wa ubunge katika jimbo la Singida Kaskazini, Songea mjini na Longido Kaskazini. Pia kata sita zinatarajiwa kufanya uchaguzi huo.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search