Droo kamili ligi ya Klabu Bingwa Ulaya hii hapa...soma habari kamili na matukio360..#share


Na mashirika ya kimataifa
VIONGOZI wa Ligi ya Premia, Manchester City watakutana na FC Basel ya Uswizi, Manchester United wakutana na Sevilla wanaocheza La Liga nao Liverpool watakutana na FC Porto ya Ureno.


Chelsea wamepangwa kukutana na Barcelona hatua ya 16 bora katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, Tottenham nao wakapewa mabingwa wa Italia Juventus baada ya droo kufanywa.

Mabingwa watetezi Real Madrid watakutana na Paris St-Germain.
Klabu tano kutoka England zilifuzu kwa hatua ya makundi msimu huu, ambayo ni rekodi.

Chelsea ndio pekee wa Uingereza waliofuzu wakiwa wa pili kutoka kundi lao, klabu nyingine zote zilimaliza kileleni.

Washindi wa makundi watakuwa ugenini mechi za kwanza 13/14 na 20/21 Februari na nyumbani mechi za marudiano mnamo 6/7 na 13/14 Machi. Fainali itachezewa Kiev mnamo 26 Mei.

Droo kamili: Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya
Juventus v Tottenham
FC Basel v Manchester City
Porto v Liverpool
Sevilla v Manchester United
Real Madrid v PSG
Shakhtar Donetsk v Roma
Chelsea v Barcelona

Bayern Munich v Beskitas

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search