Serikali yapoteza bilioni 300...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Salha Mohamed, Dar es salaam 

MWAKA 2016 Serikali imepoteza  bilioni 300 kutokana na biashara za masoko ya bima ya nje ya nchi.

Kamishna  Mamlaka ya Usimamizi wa shughuli za Bima (TIRA)  Dk Baghayo Saqware (wapili kulia)  akizungumzia uzinduzi wa waraka na:055/2017

Mkurugenzi wa Leseni na Mwenendo wa Masoko, Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima (TIRA), Samwel Mwiru ameyasema hayo  wakati wa uzinduzi wa waraka na:055/2017 wa masharti ya kufanya biashara na makampuni ya bima mtawanyo na madalali wa bima mtawanyo kutoka nje ya nchi. 

Amesema katika nchi za SADC  kiwango cha biashara ya nje asilimia 57 ya biashara ya bima inabaki ndani ya  nchi .


"Tunapungua kwa asilimia 8,mwaka 2016 fedha ambazo zilikwenda nje ya nchi ni bilioni 300,"amesema. 

Amesema kwa waraka huo unaoweka masharti ya kufanya biashara na makampuni ya bima mtawanyo na madalali wa bima mtawanyo kutoka nje ya nchi utaongeza kiwango cha biashara ndani ya nchi. 

Kwa upande wake Kamishna wa Bima (TIRA) Dk. Baghayo Saqware amesema makampuni yatakayoshindwa kufuata waraka huo hawatasita kufungia leseni zao za biashara. 

Amefafanua kuwa mamlaka ilibaini matumizi hasi ya utaratibu wa kupeleka nje biashara za bima mtawanyo kwa baadhi ya makampuni ya bima nchini. 

Amesema kuzunduliwa kwa waraka huo ni jitihada za mamlaka katika kukabiliana na changamoto zinazojitokeza kutokana na kupeleka biashara za bima nje ya nchi kupitia utaratibu wa bima mtawanyo 'reinsurance'. 

"Mamlaka ilibaini baadhi ya makampuni ya bima nchini kufanya biashara za bima na makampuni ya bima mtawanyo yasiyo na viwango bora," amesema. 

Amesema kutokana na mapungufu hayo, mamlaka imetoa waraka huo kudhibiti mwenendo hasi na kuimarisha ufanisi katika upelekaji wa biashara za bima mtawanyo nje ya soko la bima Tanzania. 

Amesema wamejidhatiti  majukumu chini ya serikali ya awamu ya tano ya John Magufuli katika dhamira ya kujenga uchumi wa viwanda kwa kutoa huduma za bima kwa wananchi na makampuni.

"Itatengeneza fursa za ajira kwa watanzania na kuongeza mchango wa sekta ya bima katika pato la taifa, "amesema. 

Waraka huo utaanza kutumika Januari mosi, 2018.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search