Mwenyekiti CCM akamatwa...soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Singida
JESHI la polisi mkoani
Singida linamshikiria mwenyekiti wa
CCM mkoa wa Singida Juma Kilimba kwa
tuhuma za kusababisha kifo cha mwanae Fatma, aliyekufa kutokana na ajali ya
gari.
Desemba 25, 2017 mwenyekiti
huyo, mkewe na watoto wao watatu walijeruhiwa baada ya gari alilokuwa akiendesha
kupinduka eneo la Msigiri wilayani Iramba mkoani Singida.
Mwenyekiti wa CCM mkoani Singida, Juma Kilimba
Kamanda wa polisi mkoani
Singida amesema upelelezi wa awali unaonyesha ajali ilitokana na ubovu wa gari
na kwamba 'steering road' ya gari hilo ilichomoka.
"Tunamshikiria
mwenyekiti huyu wa CCM, uchunguzi wa awali unaonyesha ajali ilisababishwa na
ubovu wa gari alilokuwa akiendesha hasa 'steering road' ilichomoka na
kusababisha ajali na baadae kupelekea kifo cha mtoto wake Fatma," amesema
Jumatatu ya Desemba 25, 2017
Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Jamson Mhagama alisema ajali hiyo ilitokea
mchana na Kilimba alilazwa katika
Hospitali ya Kiomboi huku mkewe Kilimba na wanawe walipelekwa katika Hospitali
ya Rufaa ya Itigi na kwamba CCM mkoani Singida inaendelea kusimamia matibabu yao.
Pia alisema mmoja kati ya watoto hao alikuwa akipatiwa
huduma katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU).
No comments:
Post a Comment