Sekretarieti maadili ya umma yatoa siku tatu kwa viongozi.....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imetoa siku tatu kwa viongozi wa umma ambao hawajatoa tamko la mali zao kufanya hivyo na watakaoshindwa watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Wapili kutoka kushoto ni Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Harold Nsekela akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Pia imewataka viongozi wa umma wastaafu kujaza fomu za tamko la rasilimali na madeni na kuziwakilisha kwa kamishna ili kujua kama mali walizonazo kwa sasa walizipata kwa halali ama la.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Maadili wa Sekretarieti Jaji Mstaafu Harold Nsekela akizungumza na waandishi wa habari, amewataka katika matamko hayo kuambatanisha na mali za wenza wao na watoto wao  umri usiozidi miaka 18.

“Kwa kuzingatia sheria ya maadili ya viongozi wa umma, kifungu cha 9 (1) (b) kinamtaka kiongozi wa umma, kila mwisho wa mwaka kupeleka kwa kamishna wa maadili tamko la maandishi katika hati rasmi linaloorodhesha mali au rasilimali zake na za mwenza wake na za watoto wake wenye umri usiozidi miaka 18 na ambao hawajaoa au kuolewa, mwisho wa kuwasilisha fomu hizo ni Disemba 30,” amesema Jaji Nsekela.

Jaji Nsekela amesema ni kosa kwa mujibu wa kifungu cha 15 (c) cha sheria ya maadili ya viongozi wa umma kwa kiongozi kushindwa kutoa tamko bila sababu ya msingi.

Naye Ofisa Sheria Mkuu wa Sekretarieti hiyo Filotheus Manula akitaja hatua ambazo zinawezakuchukuliwa kwa viongozi watakaoshindwa kutekeleza matakwa ya sheria hiyo, amesema ni pamoja na kushushwa cheo.

Nyingine ni kusimamishwa kazi, kufukuzwa kazi, mwenye mamlaka ya uteuzi anaweza kuchukua hatua stahiki na onyo kwa viongozi ambao hawana uelewa wa kutosha juu ya sheria hiyo kutokana na kutokuwa na uzoefu huo.







About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search