Jiji la Dar es Salaam lapokea tuzo ya kimataifa...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Christina Mwagala
KUPITIA mradi wa mabasi yaendayo haraka, jiji la Dar es Salaam ni miongoni mwa majiji 10 Duniani yaliyopata tuzo ya C40 Bloomberg Philantropies 2017
Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akitoa neno la shukrani baada ya kukabidhiwa tuzo ya C40 Bloomberge Philantropies .
Katika tuzo hiyo mwaka 2017 imepokelewa na Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Miwta aliyerejea nchini alfajiri ya Desemba 8, 2017.
Jiji la Dar es Salaam limechangia tuzo hiyo na Jiji la New York la nchini Marekani.
Mradi wa mabasi yaendayo haraka unawahudumia abiria 200,000 kila siku kwa kutumia mabasi ya kisasa ambayo yanachangia kupunguza msongamano wa magari barabarani na kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa na hivyo kuwa siri ya mafanikio ya tuzo hiyo.
Tuzo ya C40 Bloomberg Philanthropies hutolewa kila mwaka katika miradi inayotekelezwa kwenye maeneo mahususi matano ili kutambua jitihada za majiji wanachama wa Taasisi ya mtandao wa Majiji zaidi ya 90 duniani inayoshughulika na namna bora ya kukabiliana na Athari za mabadiliko ya Tabia ya Nchi Duniani.
KUPITIA mradi wa mabasi yaendayo haraka, jiji la Dar es Salaam ni miongoni mwa majiji 10 Duniani yaliyopata tuzo ya C40 Bloomberg Philantropies 2017
Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akitoa neno la shukrani baada ya kukabidhiwa tuzo ya C40 Bloomberge Philantropies .
Jiji la Dar es Salaam limechangia tuzo hiyo na Jiji la New York la nchini Marekani.
Mradi wa mabasi yaendayo haraka unawahudumia abiria 200,000 kila siku kwa kutumia mabasi ya kisasa ambayo yanachangia kupunguza msongamano wa magari barabarani na kupunguza uchafuzi wa hali ya hewa na hivyo kuwa siri ya mafanikio ya tuzo hiyo.
Tuzo ya C40 Bloomberg Philanthropies hutolewa kila mwaka katika miradi inayotekelezwa kwenye maeneo mahususi matano ili kutambua jitihada za majiji wanachama wa Taasisi ya mtandao wa Majiji zaidi ya 90 duniani inayoshughulika na namna bora ya kukabiliana na Athari za mabadiliko ya Tabia ya Nchi Duniani.
No comments:
Post a Comment