Kesi kigogo TRA anayemiliki gari 19, kuunguruma Januari...soma habari kamili na matukio360..#share


Na Abdulrahim Sadiki
AFISA msaidizi wa forodha wa TRA, Jennifer Mushi anayekabiliwa na mashtaka mawili ikiwamo la kukutwa akimiliki gari 19,  mali isiyolingana na kipato chake halali katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu atasomewa maelezo ya awali, Januari 11,2018.


Jennifer ameshtakiwa mahakamani hapo, chini ya kifungu cha 27, (1) (a) na (b) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11ya mwaka 2007.

Leo alipaswa kusomewa maelezo hayo ya awali  lakini Wakili wa Serikali Mkuu, Vitalis Peter ameeleza mahakamani  kuwa bado hawajamaliza kuiandaa. Hivyo aliomba ipangiwe tarehe nyingine.

Hakimu Shaidi ameiahirisha kesi hiyo hadi Januari 11,2018 ambapo mshtakiwa huyo atasomewa maelezo hayo ya awali (PH) na kesi kuanza kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kuwa  kati ya Machi 21,2016 na Juni 30,2016  jijini Dar es Salaam  akiwa  mwajiriwa wa TRA kama Afisa Forodha Msaidizi alikutwa akimili magari 19.

Nagari hayo ni   Toyota RAV4, Toyota RAV4, Toyota Dyna Truck, Toyota Viz, Suzuki Carry, Toyota Ipsum, Toyota Wish, Toyota Mark II, Toyota Wish na  Toyota Mark X.

Mengine ni Toyota Regiusage, Toyota Estimated, Toyota Alex, Toyota Noah, Toyota Crown,  Toyota Hiace, Toyota Estima, Toyota Passo na Suzuki Carry yote yakiwa na thamani ya Sh 197,601,207 Mali ambayo hailingani na kipato chake halali.

Anadaiwa kuwa, kati ya Machi  21 ,2012 na  Machi 30,2016 Dares Salaam akiwa mwajiriwa wa TRA kama Afisa Forodha Msaidizi alikutwa akiishi maisha ya kifahari  yenye thamani ya Sh 333,255,556.24 fedha ambayo hailingani na Kipato chake halali.


Baada ya kusomewa mashtaka hayo mshtakiwa huyo alikana na yupo nje kwa dhamana.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search