Makalla awapa mtihani watendaji Mbeya...soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu
IFIKAPO mwaka 2020 wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri na waganga wakuu mkoani Mbeya
wameagizwa kutekeleza sera ya afya ya jamii kwa kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na kituo cha afya na zahanati.
Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos
Makalla(katikati) akipokea mifuko 40 ya saruji yenye thamani ya milioni
5 kutoka kwa wafanyakazi wa benki ya
Akiba Commerce kwa ajili ya ukarabati wa njia ya wagonjwa katika hospitali
ya Mkoa wa Mbeya.
Agizo hilo limetolewa leo na mkuu wa mkoa huo Mkoa Amos Makalla kwenye kikao cha afya cha mkoa kilichohusisha wadau wote wa afya
kilicholenga kujadili changamoto na
mafanikio hususan mikakati ya ujenzi wa vituo vya afya na zahanati katika
kila kijiji.
"Hicho ni kipimo cha utendaji wa kazi ni lazima
mpambane kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na zahanati na kituo cha afya," amesema
Makalla.
Amesema nchi yoyote haiwezi kupiga hatua za
kimaendeleo kama wananchi wake wanakosa huduma za msingi ikiwamo ya afya na
kwamba wananchi washirikishwe kuchangia miradi
ya maendeleo.
Kaimu mganga mkuu wa hosptali ya mkoa, Dk Yahya Msuya
amesema baada ya majadiliano ya kina na wadau wa sekta ya afya wataanza ujenzi
wa vituo vya afya na zahanati katika kila kijiji.
Katika kukabiliana na hali hiyo pia kuna changamoto ya
ukosefu
wa matumizi ya vyoo bora na ni asilimia
68 tu wakazi ndio wanatumia vyoo bora.



No comments:
Post a Comment