Zanzibar Heroes yapokelewa shughuli zasimama 'Zenji'...soma habari kamili na matukio360..#share


Na Mwajuma Juma, Zanzibar
KIKOSI cha timu ya Taifa ya Zanzibar ‘Zanzibar Heroes’ kimerejea visiwani leo na kupokelewa kwa shangwe kubwa na mashabiki na wananchi wa Zanzibar.


Kikosi cha Zanzibar Heroes

Kikosi hicho ambacho kimepata nafasi ya  pili katika mashindano ya Chalenji nchini Kenya kiliwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa kwa ndege ya kukodi ya Tropical majira ya saa 6:15 za mchana.

Kikosi hicho kilichoongozwa  na Waziri wa Habari, Utamaduni Utalii na Michezo Rashid Ali Juma, kilipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Ayoub Mohammed Mahmoud.

Katika mapokezi hayo wananchi na viongozi mbali mbali walijitokeza kuja kuwalaki  kwa  kuimba nyimbo mbali mbali ikiwemo wimbo wa Sisi Sote ambao huimbwa mara nyingi wakati wa sherehe za Mapinduzi.

Msafara wa wachezaji hao ulianza katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa na kupitia Kiembe Samaki, Mwanakwerekwe, Amani na kumalizikia katika Mnara wa Kumbukumbu uliopo Kisonge mjini Unguja.

Wakati wachezaji hao wakipita katika barabara hiyo walishangiliwa kwa shangwe na wananchi waliokaa pembezoni mwa njia hizo huku shughuli nyingi za kijamii zikisita.
Timu ya Taifa ya Zanzibar ilikuwa nchini Kenya kushiriki michuano ya Chalenj ilifikia hatua ya fainali na kufanikiwa kupata nafasi ya pili kufatia kufungwa na wenyeji Kenya kwa penant  3-2 .


Timu hizo ziliweza kupigiana mikwaju ya penati baada ya kumaliza dakika 120 wakiwa sare ya mabao 2-2 hatua ambayo ilifikia hilo kutokana na kumaliza dakika 90 wakiwa sare ya kufungana bao 1-1.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search