Meya Mwita kuunguruma Addis Ababa...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Christina Mwagala, Dar es Salaam
MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar
es Salaam, Isaya Mwita anatarajia kuhutubia katika mkutano wa kimataifa wa kujadili
changamoto zinazowakabili viongozi wa serikali za mitaa.
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita
Ameondoka Jijini Dar es
salaam jana jioni kuelekea jijini Addis
Ababa, Ethiopia kunakofanyika mkutano huo.
Katika mkutano huo wa siku
tatu uliondaliwa na Umoja wa Mataifa(UN) unalengo la kujadili na kutoa majibu
ya changamoto ambazo wanakutana nazo viongozi wa serikali za mitaa wakiwamo mameya
wote.
Miongoni mwa changamoto
ambazo zitajadiliwa katika mkutano huo ni
suala la bajeti katika halmashauri na ukusaji wa mapato.
Mkutano huo pia utahudhuriwa
na viongozi wengine wa serikali za mitaa kutoka nchi mbalimbali.
Meya Mwita atazungumzia changamoto
zilizopo katika jiji la Dar es Salaam na
namna ambavyo wameweza kuzitatua.
Pia ataelezea mafanikio
yaliyopo katika jiji la Dar es Salaam kupitia sekta mbalimbali za maendeleo.
"Pamoja na mambo mengine mkutano huu utatujengea uwezo wa kiutendaji
katika shughuli zetu za kila siku," amesema Mwita.
No comments:
Post a Comment