Wakuu wa wilaya,wakurugenzi Mbeya wabanwa...soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Mbeya
WAKUU wa wilaya , Wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani hapa
wameagizwa kushirikiana na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuanza
mara moja ukaguzi wa maroli ya mizigo ili kubaini njia zinazotumika
kusafirishia chakula,dawa na vipodozi vyenye viambata vya sumu kinyemela kupitia
mpaka wa Malawi na Zambia.
Wakuu wa wilaya,wakurugenzi mkoani Mbeya wakimsikiliza mkuu wa mkoa huo, Amos Makalla hayupo pichani hii leo
Pia wakurugenzi wameagizwa kufanya operesheni ya kukagua bidhaa
zinazoingizwa katika masoko yote hususan maduka ya vipodozi ,
bucha za nyama, samaki na machinjio ya mifugo ili kubaini ubora wa
vyakula vinavyoingizwa kwa lengo la kulinda afya za watumiaji.
Mkuu wa Mkoa Amos Makalla, ametoa maagizo hayo leo , kwenye kikao
cha kujadili sheria za chakula , dawa na vipodozi kilichohusisha Wakuu
wa wilaya, Wakurugenzi ,Waganga wakuu wa wilaya, Wakuu wa Idara,
Maofisa afya na kilimo kilichofanyika katika ukumbi wa mkapa jijini
hapa.
Amesema jukumu la kufanya ukaguzi sio la TFDA pekee bali
linawahusu wote kutokana na halmshauri kukasimishwa majukumu katika
maeneo yao kufanya ukaguzi wa bidhaa zinazoingizwa na kutoka nchi
hususan dawa,chakula na vipodozi.
"Nimebaini halmashauri hamtekelezi majukumu mliokasimishwa na TFDA
sasa ninaagiza kuanzia sasa mkaanze utekelezaji wa agizo langu
hususan katika mipaka ya nchi jirani ya Zambia na Malawi kwani kuna
zaidi ya njia za kipanya 300 zinazotumiwa na wafanyabishara kuingiza
bidhaa nchini "amesema.
Meneja wa (TFDA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Rodney Alananga
amesema ushirikiano mzuri baina wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa
halmashauri mkoani hapa, utaleta tija katika kutokomeza uingizwaji wa
bidhaa kiholela.
Mkaguzi wa TFDA, Kanda , Poul Sonda alisema kufuatia changamoto ya
baadhi ya wafanyabishjara kuuza bidhaa zisizo na ubora elimu imekuwa
ikitolewa mara kwa mara na lengo ni kusaidia jamii iwe na afya bora
katika kuelekea uchumi wa viwanda.
WAKUU wa wilaya , Wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani hapa
wameagizwa kushirikiana na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuanza
mara moja ukaguzi wa maroli ya mizigo ili kubaini njia zinazotumika
kusafirishia chakula,dawa na vipodozi vyenye viambata vya sumu kinyemela kupitia
mpaka wa Malawi na Zambia.
Wakuu wa wilaya,wakurugenzi mkoani Mbeya wakimsikiliza mkuu wa mkoa huo, Amos Makalla hayupo pichani hii leo
Pia wakurugenzi wameagizwa kufanya operesheni ya kukagua bidhaa
zinazoingizwa katika masoko yote hususan maduka ya vipodozi ,
bucha za nyama, samaki na machinjio ya mifugo ili kubaini ubora wa
vyakula vinavyoingizwa kwa lengo la kulinda afya za watumiaji.
Mkuu wa Mkoa Amos Makalla, ametoa maagizo hayo leo , kwenye kikao
cha kujadili sheria za chakula , dawa na vipodozi kilichohusisha Wakuu
wa wilaya, Wakurugenzi ,Waganga wakuu wa wilaya, Wakuu wa Idara,
Maofisa afya na kilimo kilichofanyika katika ukumbi wa mkapa jijini
hapa.
Amesema jukumu la kufanya ukaguzi sio la TFDA pekee bali
linawahusu wote kutokana na halmshauri kukasimishwa majukumu katika
maeneo yao kufanya ukaguzi wa bidhaa zinazoingizwa na kutoka nchi
hususan dawa,chakula na vipodozi.
"Nimebaini halmashauri hamtekelezi majukumu mliokasimishwa na TFDA
sasa ninaagiza kuanzia sasa mkaanze utekelezaji wa agizo langu
hususan katika mipaka ya nchi jirani ya Zambia na Malawi kwani kuna
zaidi ya njia za kipanya 300 zinazotumiwa na wafanyabishara kuingiza
bidhaa nchini "amesema.
Meneja wa (TFDA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Rodney Alananga
amesema ushirikiano mzuri baina wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa
halmashauri mkoani hapa, utaleta tija katika kutokomeza uingizwaji wa
bidhaa kiholela.
Mkaguzi wa TFDA, Kanda , Poul Sonda alisema kufuatia changamoto ya
baadhi ya wafanyabishjara kuuza bidhaa zisizo na ubora elimu imekuwa
ikitolewa mara kwa mara na lengo ni kusaidia jamii iwe na afya bora
katika kuelekea uchumi wa viwanda.
No comments:
Post a Comment