TFDA kununua mitambo kudhibiti sumu kuvu...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara

MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA) ipo katika mikakati ya kupata  mitambo ya kisasa ya kuchunguza sumu kuvu ili kulinda afya za watumiaji wa nafaka hasa mahindi.

Mkurugenzi  mkuu wa TFDA, Hiit Sillo 

Sumu kuvu ni aina ya kemikali za sumu inayozalisha ukungu au fangasi kwenye mbegu za nafaka kama mahindi, kunde na karanga.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi mkuu wa TFDA, Hiit Silo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufunga mkutano wa siku mbili uliwakutanisha wataalam kutoka nchi 15 za Afrika.


Lengo la mkutano huo lilikuwa ni kujadili mikakati ya kudhibiti sumu kuvu katika nafaka.

“Kwa sababu kama ambavyo taarifa za nyuma zimetolewa ni kwamba huwezi kutazama mahindi na kusema kwamba yana sumu kuvu lazima uwe na uwezo wa kuchunguza,” amesema Sillo.

Sillo amesema kutokana na athari za sumu kuvu kwa afya ya binadamu, TFDA imechukua hatua mbali mbali ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara na umuhimu wa kutunza mahindi ili kuepukana na maradhi yatokanayo na tatizo hilo.

Mkurugenzi wa usalama wa chakula wa TFDA, Raymond Wigenge ameanisha  mambo manne  yanayotegenezewa  miradi kwa ajili ya utekelezaji.

Mambo hayo ni uelimishaji jamii, teknolojia, tafiti mbalimbali, na sera mahususi zinazolenga kushughulikia tatizo.


Wigenge amesema mazingira yenye unyevunyevu ni rahisi kuzalisha fangasi  wanaosababisha t sumu kuvu na amewataka wananchi kuhifadhi nafaka katika mazingira makavu.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search