Mambosasa awataka polisi kuwa 'nga'ng'ari'...soma habari kamili na matukio360..# share

Na mwandishi wetu
KAMANDA wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amewasisitiza askari kufanya mazoezi ya viungo.

Askari polisi kanda maalum ya Dar es Salaam wakifanya mazoezi.

Amesema  hayo leo aliposhiriki katika matembezi na mazoezi ya viungo na askari wa vikosi vya kanda maalum ya Dar es Salaam.

“Askari na jamii kwa ujumla wanapaswa kufanya mazoezi  pale wanapopata nafasi na sio mpaka walazimishwe kwani mazoezi yanasaidia kujenga mwili na kuuepusha mwili na magonjwa kama vile presha na kisukari,” amesema,

Awali Kamanda  Mambosasa aliwapongeza askari kwa kushiriki mazoezi hayo, amesema mazoezi hayo yatakua endelevu kwa askari wote wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam .


Matembezi hayo ya root match yalifanyika katika mikoa ya kipolisi Temeke na Kinondoni na yatakuwa yakifanyika kila jumamosi ya mwisho wa mwezi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search