Makonda ateuliwa tena...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewateua mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda na mkurugenzi mkuu wa makampuni ya Bakhresa Limited, Abubakar Bakhresa kwenye kamati za maandalizi ya fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 (AFCON U-17) yatakayofanyika 2019 nchini.
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewateua mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda na mkurugenzi mkuu wa makampuni ya Bakhresa Limited, Abubakar Bakhresa kwenye kamati za maandalizi ya fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 (AFCON U-17) yatakayofanyika 2019 nchini.
Rais wa TFF Wallace Karia
Katika uteuzi huo Makonda ameteuliwa
kuwa mwenyekiti wa kamati ya miundombinu huku Bakhresa akiteuliwa kuwa makamu
mwenyekiti wa kamati ya usafiri na malazi.
Kwa mujibu wa rais wa TFF, Wallace
Karia, Makonda atasaidiwa na makamu mwenyekiti Yusuph Singo ambaye pia ni
mkurugenzi wa michezo.
Wajumbe katika kamati ya miundumbinu
ni Sunday Kayuni, Leslie Liunda, Nassoro Idrissa ‘Father’, Mohamed Kiganja katibu
wa baraza la michezo la taifa (BMT) na Mhandisi Davis Shemangale.
Kwa upande wake Bakhresa atakuwa chini
ya mwenyekiti mhandisi Ladislaus Matindi na wa kamati hiyo ni Aziz Abood, Ahmed Mgoyi, Ahmed Shabiby, Dk.
Maige Mwakasege Mwasimba na Shebe Machumani.
TFF pia imeunda kamati ya masoko na mabari
chini ya Mwenyekiti, Kelvin Twissa na Wajumbe Mwandishi wa Habari za Michezo na
Katibu wa zamani wa TFF, Angetile Osiah, Mkurugenzi wa Idara ya Habari
(MAELEZO), Dk. Hassan Abbas, Dk. Omari Swaleh wa Chuo Kikuu cha Mzumbe,
Mkurugenzi wa AMG Group Iman Kajula na Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited,
Tido Mhando.
Kamati nyingine ni ya Fedha na Mipango
itakayokuwa chini ya Mwenyekiti, Doto James na Wajumbe Mohamed Dewji, Dk. Seif
Muba, Bernard Lubogo, Paul Bilabaye, Jacquelline Woiso na Cornel Barnabas.
Kamati ya Uratibu Utalii itakuwa chini
ya Mwenyekiti, Dk Khamis Kigwangala na Wajumbe , Allan Kijazi Devotha Mdachi
ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Temeke, Hoyce Temu, Leah Kihumbi
ambaye ni Mkurugenzi wa Sanaa na Makamu Rais wa zamani wa TFF, Athuman
Nyamlani.
Kamati ya Itifaki, Mwenyekiti ni
Mndolwa Yusuph ambaye ni Kamishna Mkuu wa Uhamiaji na Wajumbe Filbert Bayi,
Mkurugenzi Uwanja wa Ndege JNIA, Happiness Luangisa, Alex Makoye Nkenyenge na
Alhaji Idd Mshangama.
Kamati ya Tiba na Udhibiti wa Dawa za
Kusisimua Misuli itakuwa chini ya Mwenyekiti, Profesa Lawrence Museru, Dk. Paul
Marealle, Dk. Edmund Ndalama, Dk. Christina Luambano, Daktari Mkuu wa Hospitali
ya Temeke na Hiiti Sillo.
Kamati ya Sheria na Taratibu
Mwenyekiti ni William Erio na Wajumbe Dk. Damas Ndumbaro, Edwin Kidifu, Ally
Mayai na Khalid Abeid.
Kamati ya Ulinzi na Usalama Mwenyekiti
ni IGP Simon Siro na Wajumbe Michael Wambura, CP. Andengenye wa Zimamoto,
CP. Lazaro Mambosasa wa Polisi Kanda Maalum ya Dar-es-Salaam, Mkuu wa Askari wa
Usalama Barabarani, TISS na Jonas Mahanga.
Kamati ya Rasilimali Watu itakuwa
chini ya Mwenyekiti Dk. Francis Michael, Allan Kijazi, Wane Mkisi, Juliana
Yassoda na Gerald Mwanilwa.
Kamati hizo ndogo zitakuwa chini ya
Kamati Kuu inayoongozwa na Mwenyekiti Dk. Harrison Mwakyembe (MP); Makamu
Mwenyekiti wa Leodegar Tenga na Mtendaji Mkuu wa Kamati hiyo ni Henry B.
Tandau.
No comments:
Post a Comment