Mamilioni ya dola yaliibwa katika mazishi ya Mandela...soma habari kamili na matukio360..#share

Na mashirika ya kimataifa
MIAKA minne tangu kufarika kwa aliyekuwa  rais wa zamani wa Afrika kusini, Nelson Mandela imebainika viongozi wakuu nchini humo wanadaiwa kufanya ufisadi mkubwa katika mazishi ya kiongozi huyo.

Hayati Nelson Mandela rais wa zamani wa Afrika Kusini

Mamlaka ya kupambana na rushwa nchini humo imebaini kuwa takriban dola milioni 22 ilitumika vibaya wakati wa matayarisho ya mazishi ya Mandela miaka minne iliyopita.

Ripoti hiyo inasema kwamba viongozi hao walifuja pesa na kukiuka taratibu zilizowekwa huku ikisemekana kwamba gharama za bidhaa ziliongezwa maradufu na matumizi mazishi kutajwa kuwa ya juu sana kwa mfano shati za kumbukumbu ya mazishi zilinunuliwa kwa dola 25 badala ya dola 19 .

Hata hivyo ripoti hiyo imetaka hatua kali kuchukuliwa dhidi ya wahalifu waliofanya jambo hilo la kushangaza katika jamii.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search