Waziri Kalemani :Hakuna mgawo wa umeme...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu
WAZIRI wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema  hali ya umeme kwa sasa ni wastani na hakuna mgao.

Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani

Amesema hayo katika kipindi cha tunatekeleza  na kusema “ Si kwamba tuna mgao wa umeme, tunarekebisha mitambo ya umeme iliyodumu kwa takribani miaka 40.”

Amesema lengo ni kuhakikisha kunakuwapo na mitambo ya umeme itakayowezesha kutoa huduma ya umeme kwa uhakika na kuwa umeme ni uchumi na huwezi kutenganisha masuala ya maendeleo na nishati.

Waziri hiyo amesema  upungufu wa umeme unatokana na ukarabati unaoendelea na mafundi hawalali kuhakikisha hali inakuwa sawa.

“Hadi kufikia Desemba 15,2017 tutakuwa tumefanya ukarabati katika sehemu kubwa na kutakuwa na tofauti kubwa,’’ amesema

Pia amesema  hadi kufikia mwezi wa 1 au wa 2, 2018  mkandarasi wa  kujenga stiegler's gorge atapatikana  na kuanza ujenzi. Mradi wa stiegler's gorge utazalisha megawati 2100 kwa mkupuo.

Amesema mradi wa Kinyerezi 2 umekamilika kwa 86% na kuanzia mwezi huu utaanza kutoa  megawati 30 kila mwezi.

Mradi wa umeme Makambako-Songea ni mradi mkubwa utakuwa na vituo 3 vya kupoozea umeme, utakamilika Septemba mwakani.

Waziri huyo amesema katika REA 3 serikali itahakikisha kila kijiji kinapata umeme na kwamba vijiji zaidi ya 7,000 havijapata umeme


"Mpaka kufikia mwaka 2021 vijiji vyote vitakuwa vimepata umeme,’’ amesema

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search