Marekani yaibembeleza Korea Kaskazini...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
WAZIRI wa mambo ya nje wa Marekani, Rex Tillerson amesema nchi yake ipo tayari kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na Korea Kaskazini bila ya masharti yoyote.
Rex Tillerson, Waziri wa mambo ya nje wa Marekani
Amesema lengo kuu la mazungumzo hayo ni kuweka mambo sawa na kufikia makubaliano yenye amani bila kuwepo kwa vita.
Tillerson ameonya kuwa mazungumzo hayo yatafanyika tu iwapo Korea Kaskazini itasitisha majaribio yake ya makombora ya nyuklia.
Ameitaka Korea Kaskazini kurejea katika meza ya mazungumzo.
"Tupo tayari kwa mazungumzo muda wowote na Korea Kaskazini,tena mazungumzo yasiyo na masharti.Hebu tukutane.Hatuwezi kuzungumzia namna mpangilio wa mazungumzo hayo,utakavyo kuwa kama ni meza ya duara ama la,Lakini je tunaweza kukaa chini uso kwa uso tujadili jambo hili?na kisha kuanza kuweka namna ya kufikia maridhiano. "
Rex Tillerson amekuwa akifanya kila linalowezekana kusaka suluhu ya mzozo wa taifa lake na Korea Kaskazini kwa njia ya majadiliano na si vita.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search