Mbunge Lijualikali na Susan Kiwanga waendelea kusota rumande..soma habari kamili na matukio360...#share

PETER Lijualikali na Suzan Kiwanga wabunge wa Kirombelo na Mlimba wote kwa tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na wenzao 36 wamerejeshwa rumande.
P Lijualikali na Suzan Kiwanga 

Wabunge hao na wenzao leo wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro ambapo mahakama ilitakiwa kutoa uamuzi wa dhamana lakini umekwama kutokana na kuibuka hoja za kisheria.

Kulitokea mvutano kati ya upande wa mashtaka na ule wa utetezi kuhusu hati ya kiapo ya kupinga dhamana iliyowasilishwa mahakamani hapo.

Kutokana na mvutano wa kisheria, hakimu Ivan Msack ameahirisha kesi hiyo hadi kesho Jumatano Desemba 6,2017 ili kutoa fursa kwa pande zote mbili kujibu hoja kuhusu hati hiyo.

Washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka nane likiwamo la kuchoma moto ofisi ya Kata ya Sofi iliyopo wilayani Malinyi.

Washtakiwa wanatetewa na mawakili Peter Kibatala, Ignas Punge, Fredrick Kiwelo na Bartholomew Tarimo.
Upande wa mashtaka unawakilishwa na mawakili wa Serikali, Edga Bantulaki na Sunday Hyera.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Frederick Sumaye walihudhuria mahakamani.


Wengine waliofika mahakamani ni mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na wa Viti Maalumu, Devota Minja.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search