Mume, mke kizimbani kwa Heroin gram 375...soma habari kamili na matukio360..#share


Na Abdulrahim Sadiki
MUME na mke ambao ni wafanyabiashara wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa kusafirisha  dawa za kulevya aina ya Heroin  gram 375.20.



Akisoma hati ya mashtaka leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, Wakili wa Serikali, Adolf Mkini amewataja washtakiwa hao kuwa ni  Minda Mfamai, mkewe  Fatuma Mpondi na  mwenzao Oswini Mango.


Wakili Mkini amedai Novemba 22, 2017 katika maeneo ya Chamazi kwa Mkongo Mbagala, wilayani Temeke,  Dar es Salaam washtakiwa hao walisafirisha madawa hayo.

Baada ya kusomewa shtaka hilo, washtakiwa  hawakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu.

Hakimu Mashauri ameiarisha kesi hiyo hadi Desemba 19,2017 na kuamuru mshtakiwa Minda akatibiwe baada ya kulalamika kuwa alipigwa alipokuwa  polisi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search