Wanaotumia ARvs Dodoma waongezeka... soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu, Dodoma
TAKRIBANI  wagonjwa kati ya 100  hadi 1200 wanaotumia dawa za kufumbaza maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi(ARvs) mkoani Dodoma, kwa siku hupokea dawa hizo.

Pia idadi ya wanaotumia dawa hizo imeongezeka kutoka  wagonjwa 3,144 hadi 6,244. Kati ya hao wanawake ni 4876.

Waziri wa afya, Ummy Mwalimu

Mtakwimu wa  hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma, Venance Makuza ameiambia matukio360 kuwa takwimu hizo ni za kipindi cha April hadi Septemba 2017.

Amesema ongezeko hilo ni kutokana na  mwamko wa jamii kupima afya hususan wageni wanaoingia na kutoka katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.

 â€œKwa siku  tunatoa dawa za kufubaza virusi vya ukimwi(ARvs) kwa wagonjwa 100 hadi 1200  licha ya wengine kutoudhuria kliniki kwa sababu zisizokuwa za msingi za mila, desturi na Imani za kidini,’’ amesema

Mkuu wa kitengo cha  maambukizi mpya ya virusi vya Ukimwi (HIV) mkoani humo, Dk Silaji Shaban amesema idadi kubwa ya wanawake  ni kutokana na mwamko wao wa  kujitokeza kupima afya na kupata ushauri nasaha.

"Pamoja na mambo mengine changamoto tunayokabilina nayo ni baadhi ya wagonjwa kuacha tiba kwa sababu mbalimbali ikiwemo  kukosa tendo la ndoa na imani za kidini, mira na destuli ,"amesema

Katika hatua nyingine Dk Shaban ameonya wagonjwa wanaotumia(ARvs) kuacha tabia ya ulevi wa pombe na kwamba inachangia usugu wa dawa na hatari ya kupata ugonjwa wa ini


Msimamizi wa kitengo cha utoaji dawa za ARvs, Sylvester Lugia amesem elimu ya uhamasishaji jamii kupima afya inabidi iongezeke na waathirika kuzingatia ushauri wa wataalam wa afya ili kuongeza siku za kuishi.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search