Mfumuko wa bei nchini wapungua...soma habari kamili na matukio360...#share

Na  Mwandishi Wetu

MFUMUKO wa bei  mwezi Novemba, 2017 umepungua hadi asilimia 4.4 ikilinganishwa na asilimia 5.1 mwezi Oktoba, 2017.
Mkurugenzi wa sensa ya watu na takwimu za jamii kutoka ofisi ya taifa ya takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
  

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam mkurugenzi wa sensa ya watu na takwimu za jamii kutoka ofisi ya taifa ya takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo amesema kupungua kwa mfumuko wa mwezi Novemba, 2017 kumechangiwa  na kupungua kwa bei za baadhi ya bidhaa za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Novemba, 2017 ikilinganishwa na bei za mwezi Novemba, 2016.

“Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei ni nyama ya ng’ombe asilimia 5.4, samaki wabichi asilimia 22.2, mbogamboga asilimia 3.9, viazi mviringo asilimia 14.0, mihogo mibichi asilimia 24.8 na viazi vitamu kwa asilimia 13.4,” amesema.

Amesema mfumuko wa bei nchini unamwelekeo unaofanana na baadhi ya nchi nyingine za Afrika Mashariki, nchini Kenya mfumuko wa bei mwezi Novemba, 2017 umepungua hadi asilimia 4.73 kutoka asilimia 5.72 mwezi Oktoba, 2017 na nchini Uganda umepungua hadi asilimia 4.0 mwezi Novemba, 2017 kutoka asilimia 4.8 mwezi Oktoba, 2017.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search